Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na mimi nijielekeze moja kwa moja kwenye migogoro mbalimbali iliyopo katika Jimbo langu la Mikumi ambapo pamoja na mimi mwenyewe kuileta kwenye Ofisi ya Waziri wa Ardhi mkono kwa mkono lakini cha kusikitisha ni kuwa sio tu kwamba haijaorodheshwa kwenye kitabu cha Waziri alicholeta na kukigawa kwa Wabunge, lakini pia migogoro hiyo haijatajwa kabisa mahali popote.
Naomba Mheshimiwa Waziri akija kwenye majumuisho anipe majibu ni lini na ni nini hatma ya migogoro hii ya ardhi na mashamba pori yafuatayo ambayo yapo kwenye Jimbo la Mikumi na kusababisha Watanzania wenzetu wazalendo kukosa ardhi na nyingi kupewa wanaoitwa wawekezaji ambao wameyafanya mashamba pori na mengine kuyabadilisha matumizi.
(i) Kata ya Mikumi - mgogoro kati ya wananchi wa Kitongoji cha Vikweme na JWTZ na wananchi wa Kikwalaza na Hifadhi.
(ii) Kata ya Ruhembe – mgogoro wa wananchi wa Kitete Msindazi na Hifadhi; wananchi wa Ruhembe na Hifadhi; wananchi wa Kielezo na Hifadhi na wananchi wa kijiji cha Kidogobasi na wavamizi wa ekari 98.
(iii) Kata ya Kilangali - mgogoro wa muda mrefu kati ya Kijiji cha Kilangali na Kijiji cha Tindiga; mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Mbamba na Kijiji cha Kiduhi ni wa muda mrefu sana; mgogoro wa kijiji cha Kilangali na Shamba la Mbegu la ASSA, huu nao ni wa muda mrefu sana na mgogoro wa wakulima na wafugaji kwenye Kata nzima ya Kilangali.
(iv) Kata ya Uleling‟ombe - kuna mgogoro mkubwa sana kati ya wananchi wa Uleling‟ombe na Msitu wa Ukwiva ambapo eneo hili lilihamishwa mpaka mwaka 1972 na wananchi wanaomba warudishiwe mpaka wa zamami (awali) wa mwaka 1957 ili wapate maeneo ya kulima na kujiletea maendeleo.
(v) Kata ya Ulaya - mgogoro wa ardhi kati ya Basso Masumin na Serikali ya Kijiji cha Ng‟ole; mgogoro wa ardhi kati ya wafugaji na wakulima wa Kijiji cha Mbuyuni; mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Ng‟ole na Mbamba; mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Ng‟ole na Ulaya Kibaoni, mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Ng‟ole na Mhenda na mgogoro wa mpaka kati ya Kijiji cha Ng‟ole na Nyalanda.
(vi) Mgogoro mkubwa wa shimo la mchanga kati ya Kata ya Ruaha na Kata ya Ruhembe (Kijiji cha Kitete).
(vii) Mgogoro wa ardhi kati ya Kijiji cha Kitundueta (Mhenda) na Kijiji cha Ihombwe kilichopo Mikumi.
(viii) Kata ya Kidodi - mgogoro wa mipaka kati ya Kijiji cha Lumango na hifadhi.
(ix) Kata ya Tindiga - mgogoro mkubwa sana na unaopoteza maisha ya Watanzania wengi sana kati ya wakulima na wafugaji na umedumu kwa muda mrefu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho napenda Mheshimwa Waziri atuambie ni lini mashamba makubwa yaliyotelekezwa na wanaoitwa wawekezaji yatarudishwa kwa wananchi. Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ilileta orodha ya mashamba pori 38 kwenye ofisi ya Waziri wa Ardhi bila mafanikio. Baadhi ya mashamba hayo ni:-
(i) Kata ya Kilangali - shamba Na.120 la Kivungu.
(ii) Kata ya Kisanga - shamba la SAS (Kisanga).
(iii) Kata ya Masanze - shamba la Miyombo; shamba la Dodoma Isanga na shamba la Changarawe.
(iv) Kata ya Ulaya - shamba la Ulaya.
(v) Kata ya Tindiga - shamba la Sumagro.
(vi) Kata ya Ulaya - shamba la Nyaranda
(vii) Shamba la Kilosa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu kilicholetwa na Mheshimiwa Waziri hakina takwimu shahihi ukilinganisha na hali za mashamba pori hayo yaliyopo Jimboni Mikumi. Tunaomba sana Mheshimiwa Waziri aje mwenyewe Jimboni Mikumi ili ashuhudie mapori makubwa yasiyoendelezwa wala kulimwa kama ambavyo amepewa taarifa na kusababisha wananchi wengi kukosa sehemu za kujiletea maendeleo na kuleta tija na maendeleo kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasisitiza sana naomba Mheshimiwa Waziri anipe ahadi ya kwenda pamoja na mimi Jimboni Mikumi ili akajionee mwenyewe. Ahsante sana, naomba kuwasilisha.