Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la umbali wa mita 60 kutoka ufukwe wa bahari, kingo za mito, mialo ya maziwa, maeneo yote tengefu na maeneo hatarishi (hazardous land) yazingatiwe kama sheria zinavyotaka. Kwa mujibu wa section 7(1)(d) of Land Act No. 4 of 1999 au section 7 kwa ujumla wake inaelezea kwa kirefu namna ya kuyabaini na kuyatangaza katika Gazeti la Serikali. Naomba Wizara isiishie hapo, waweke alama inapoishia mita 60 kama walivyofanya TANROADS na TANESCO wameweka vigingi vya zege kuonyesha mwisho wa mipaka ya maeneo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo yote ya wazi kwa mujibu wa cadastral surveys wapewe watu vibali siyo hatimiliki kama waangalizi. Kwa kibali maalum cha Wizara wataruhusiwa kufanya beautification kama kupanda maua (lawn grasses), kutengeneza miundombinu ya kuchezea watoto kama bembea na kadhalika. Tahadhari wasijenge majengo ya kudumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo yote yaliyotengwa kwa taasisi kama viwanja vya kujenga majengo ya shule, nyumba za ibada, mabenki, vituo vya polisi na huduma nyingine kama vituo vya mafuta, Wizara au Halmashauri zihakikishe unawekwa utaratibu kila mwananchi ayatambue maeneo haya na wawe walinzi wa maeneo haya yasivamiwe. Vichimbiwe vibao vikitaja maeneo haya ili ku-prohibit uvamizi wa maeneo haya.