Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampongeza sana Waziri kwa hotuba nzuri kuhusu sekta ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi. Pili, naunga mkono kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-
(i) Wananchi waelimishwe kuhusu matumizi bora ya ardhi na kutambua mipaka yao ya ardhi wanayoimiliki.
(ii) Wananchi wanapata shida kutembea mwendo mrefu kufuata Baraza la Ardhi. Nashauri Serikali ianzishe Baraza la Ardhi kila Wilaya ikiwemo Wilaya ya Mpwapwa na Kongwa.
(iii) Wawekezaji wasichukue ardhi ya wananchi bila kulipa fidia.
(iv) Kwa kuwa Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa hukopa fedha kwa ajili ya kupima viwanja ni vema warejeshe mikopo hiyo mapema ili Halmashauri zingine nazo zikope (revolving fund).
(v) Serikali isimamie ujenzi holela wa miji yetu (squatters) na kila mji lazima uwe na master plan kabla ya kuanza kujenga.
(vi) Serikali itenge fedha za kutosha za ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo badala ya kutegemea wafadhili ambapo hakuna uhakika wa kuletewa fedha zote.