Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuchangia kuhusu shamba la Malonje. Ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa shamba la Malonje kati ya wananchi na mwekezaji? Mgogoro huu umekuwa ni wa muda mrefu, wananchi wameteseka kwa kukosa ardhi ya kulima. Naomba Mheshimiwa Waziri atoe maelezo kuna maeneo kadhaa yenye migogoro Waziri huyu ameimaliza huu unamshindaje au kuna mikono ya wakubwa? Naomba maelezo kwani wananchi wamechoka na ahadi ambazo zimekuwa zikitolewa na Serikali. Naomba Serikali imalize haraka mgogoro huu kuepusha shari inayoweza kutokea. Ahsante.