Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Na mimi naungana na wenzangu kuendelea kumpongeza Waziri na Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara ya Ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina machache lakini sitaweza kumaliza ila nianze tu na yale ambayo ni muhimu zaidi. Kwenye ukurasa wa 43 kwenye kile kifungu cha 58 kazi mojawapo au shughuli aliyotuambia ni pamoja na programu ya Taifa ya kurasimisha na kuzuia ujenzi holela mijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sizungumzii hayo anayokwenda kufanya nazungumzia miji ilivyo sasa hivi. Ni kweli miji yetu ilikuwa imepangwa hasa ili miji ya awali kwamba kuna maeneo ya residential, industrial areas, miji na kadhalika. Kilio changu ni hali tuliyofikia sasa, eneo kama Oysterbay ni residential area lakini sasa unakuta Oysterbay kumekuwa ndiyo kwenye pubs, vilabu, ndiyo kwenye kelele usiku na mchana, Oysterbay. Leo Mwalimu angefufuka angesema nini? Sasa sijui jinsi gani yeye Waziri ambaye anashughulikia makazi analizungumzia hili na anafanya nini ili Halmashauri zisiruhusu kujenga hivyo? Sasa hivi Oysterbay hakukaliki, ni fujo tupu. Namuomba Waziri huyu mhusika aweze kuona ni jinsi gani sasa watu watalala usiku na kuamka mapema wakafanye kazi zao. Oysterbay na kwingineko kumeharibika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu huu Mji wa Dodoma, ni mji mtarajiwa kuwa Mji Mkuu au Jiji la Taifa, lakini kuko hovyo, Dodoma haijakaa namna hiyo na Dodoma ndiyo yenyewe yenye Capital Development. Iweje watu wa Nigeria walivyokuja huku, walichukua zile ramani zetu wakati wakitaka kuhamisha Lagos kwenda Abuja, wameweza kutekeleza, mji ule umehama na ni kuzuri tu. Si kweli kwamba hawa Mawaziri wetu hawajasafiri, kabla hujatua nchi yoyote ndege ikianza kutua unaona miji ilivyopangika, kwa nini wanakwenda tu wanang‟azang‟aza macho hawatuletei huo ujumbe. Sasa hivi Lagos imeshahamia Abuja na kumepangika, kwa nini siyo Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nalotaka kuzungumza ni makazi ya watu wa kawaida. Ni miaka mingapi sasa, hamsini na ya uhuru bado watu wanaishi kwenye tembe, zile nyumba ambazo tukiwa tunakuja Dodoma tunaziona, bado watu wanaishi kwenye makuti, bado watu wanaishi kwenye nyumba ambazo hata huwezi kujua kama bado tuko Tanzania. Mabati yameshushwa bei watu wajenge nyumba nzuri, haiwezekani, Waziri mhusika anasemaje, anatoa semina lini kwa watu walio vijijini wajue maana ya kuishi katika nyumba bora? Tunataka kuona anatoa semina, watu waishi kwenye nyumba zenye mabati, zenye kuta nzuri na wasaidike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua muda ni mfupi sana na nakosa amani kabisa kwa vile hakika ni mambo mazuri ningetaka kuongea lakini nizungumzie mkoa wangu. Mkoa wa Kilimajaro sasa hivi hatuna tena mahali pa kuishi vihamba vimegawiwa limebakia eneo la makaburi tu. Naomba huyu Waziri wetu kila inapowezekana tuonyeshwe eneo jipya ili vijana wetu wahamie huko sasa wakaweke makazi mapya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kuhusu Dodoma, tulikuja lile Bunge la Tisa tukakuta viwanja vimepangwa ukutani tukajichagulia viwanja, tumepelekwa Itega, mpaka leo kule Itega hawajapeleka maendeleo. Mimi ni mmojawapo ambaye nimeathirika, nilinunua kiwanja shilingi milioni nne lakini nakwendaje kujenga Itega, hakuna juhudi zozote za kuwezesha watu kujenga makazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nizungumzie National Housing. Ni Shirika ambalo limefungua watu macho na hata hapa Dodoma wakaone ghorofa za Medeli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.