Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Naomba niende moja kwa moja, niunge mkono hoja ambayo imeletwa leo hapa mbele yetu na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Waziri Lukuvi na Naibu Waziri kwa kazi kubwa wanayoifanya kuongoza na kusimamia wizara hii nyeti. Matunda ya kazi yao kweli yanaonekana, hongereni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, personally naomba nimshukuru Mheshimiwa Lukuvi kwa kuwa mfano wa kuigwa hasa kwangu mimi nikiwa kijana kiongozi. Amedhihirisha ni jinsi gani tunatakiwa kuwajibika pale tunapopewa majukumu yetu, ahsante sana Mheshimiwa Lukuvi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Ardhi ya kuhakikisha Watanzania wanapata hati zao na kutatua hii migogoro inayojitokeza katika maeneo mbalimbali, napenda kushauri suala la elimu ya ardhi litiliwe mkazo. Watanzania lazima watambue haki na thamani ya ardhi yao. Hili limekuwa ni tatizo kubwa linaendelea kujitokeza hususan kwenye Mkoa wangu wa Iringa. Kumekuwa na wajanja wachache ambao wanafika kwenye maeneo ya vijijini na kuwashauri hawa wanavijiji kuwauzia haya maeneo, moja kwa bei ya chini na pili wengine wamediriki kuwashawishi hadi kuuza maeneo yao yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotokea hawa wanavijiji wanakosa hata maeneo ya kuzalisha mazao ambayo yanaweza kuwasaidia wao kuendelea kupambana na kukidhi mahitaji ya familia zao. Kwa hiyo, hili suala la elimu Mheshimiwa Lukuvi naomba tulipe kipaumbele sana. Hii elimu isitoelewe tu kwa wale wanakijiji lakini hata hawa wawekezaji wanaokuja kununua haya maeneo kule vijijini waambiwe kuwa wanapopewa yale maeneo wahakikishe hawa wananchi wanaachiwa eneo ambalo wataendelea kuzalisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nakazania hii elimu? Tumesema tunataka Tanzania sasa iwe nchi ya viwanda na wote tulikubaliana kuwa hawa wakulima wadogo wadogo, hii asilimia 75 ambao wako kijijini wanaotegemea kilimo ndiyo wangetumia hiki kilimo kuzalisha raw materials ambazo zitapelekwa kwenye hivi viwanda. Kama haya maeneo yote yatakuwa yamebebwa na hawa watu chache, tutakapoanzisha hivi viwanda watakaonufaika ni wale ambao watakuwa na maeneo makubwa ya kuzalisha hizi raw materials na hii dhana nzima ya kuwasaidia hawa wakulima wadogo wadogo waweze kufikia ule uchumi wa kati itakuwa ni vigumu kufikiwa. Kwa hiyo, naendelea kusisitiza lazima suala la elimu lipewe kipamumbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la hati miliki hasa hizi za kimila limechangiwa kikubwa sana na Wabunge hapa ndani na mimi ningependa niongezee. Naomba hizi hati miliki za kimila zipewe uzito na ziwe zinatambuliwa kisheria. Hata nchi za wenzetu zilizoendelea, mtu anayemiliki ardhi anapewa heshima kubwa na hiyo heshima inatokana na kuwa ile hati yake popote anapokwenda, hata kwenye hizi financial institutions anaweza kukopesheka lakini hapa nyumbani kwetu bado ni changamoto kubwa sana hususan kwa wanawake. Sisi ni asilimia kubwa hapa nchini, population yetu ni zaidi ya asilimia 51 lakini ni asilimia 19 tu…
MWENYEKITI: Ahsante, kwa heri, dakika tano zako zimekwisha mlikubaliana kugawana dakika na mwenzako Mheshimiwa Juliana Shonza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niunge mkono hoja, ahsante sana.