Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia uhai na afya njema niweze kuchangia katika Wizara hii na pia napenda kukishukuru chama changu, Chama cha Wananchi CUF kwa kuniamini kunipa majukumu haya mazito. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile napenda kuishauri Serikali, kwanza na-declare interest kwamba mimi nilikuwa mfanyakazi wa ardhi na ni mtaalam wa ardhi pia. Napenda kuishauri Serikali juu ya kupima maeneo ya umma, maeneo ya umma kwa kiasi kikubwa yanavamiwa sana. Maeneo ya umma kama shule, zahanati, maeneo kama ya polisi, majeshi, hasa kwa Mkoa wa Dar es Salaam ni tatizo kubwa sana, wananchi wanaingilia maeneo haya kwa kasi kubwa sana kwa sababu hayana dermacation, hayana alama yoyote ambayo ya kueleza kwamba, hii shule inaishia hapa, kituo cha polisi kinaishia hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naiomba Wizara ifanye mkakati mzito wa kuyatambua haya maeneo ya umma kwamba yawekewe alama mahsusi na yapate hatimiliki kabisa kuepuka migogoro hii ambayo ni mizito. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile niongelee upungufu wa wafanyakazi wa sekta ya ardhi. Kwa kweli wafanyakazi wa sekta ya ardhi ni wachache, yaani wachache mno na Waziri mwenyewe analitambua hilo. Kuna Wilaya nyingi sana hazina hawa wataalam wa ardhi kabisa. Yaani unakuta hizi kazi za ardhi zinafanywa na ma-layman ambao hawana utaalam wowote na hiyo inapelekea kutokuweka mikakati ya Serikali kwamba ukiangalia Chuo Kikuu ya Ardhi ni kimoja mpaka leo, toka mwaka 1961 chuo kikuu ni kimoja! Ma-graduates wanao graduate pale hawatoshi na hata vile vile ukiangalia uajiri, Serikali kuajiri hawa wafanyakazi wa sekta ya ardhi hawaajiri kwa kasi kubwa, bado hao hao wachache, wanaendelea kukaa mitaani miaka mitatu minne mpaka kuja kuajiriwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri waweke kipaumbele kwamba hawa watu waajiriwe sana na hivyo vyuo pia viongezeke, ikiwezekana tuwe na vyuo viwili vya ardhi, mpaka vitatu ili kuangalia hili tatizo kubwa la upungufu wa wafanyakazi hawa wa ardhi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kwenye migongano ya kisera, migogoro mingi inatokana pia na migongano ya kisera, kwa mfano unakuta kwamba ile kutoa hatimiliki kwenye eneo moja; labda Jiji linatoa hatimiliki, Halmashauri zinatoa hatimiliki lakini hiyo sasa hivi angalau imerekebishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunaangalia kuna migongano kama hii ya wakazi ya mabondeni. Wale wanawatuhumu kwamba wako mabondeni lakini wana hatimiliki wale, wana zile wanaita leseni za makazi ambao anayesaini ni Assistant Commissioner wa Halmashauri na unakuta zile leseni wamechukulia mikopo. Kwa hiyo, pale wameleta mgongano kati ya mwananchi na benki kwa kwenda kumvunjia lile eneo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna hiyo migongano ya kisera sana kwamba wanatoa zile hati lakini hawaangalii je, tunapotoa kuna uhalali wa kiasi gani? Ile ni hati halali na benki wanaitambua na Wizara wenyewe wanaitambua kwa maana ni Assistant Commissioner wa Halmashauri ndiye amesajili zile hati. Kwa hiyo, huo mgongano wa kisera unafanya kwamba kuleta mgogoro mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile niangalie tena Mabaraza ya Ardhi, Mabaraza haya ya Ardhi kweli yanaisaidia Wizara kwa kiasi cha kutosha lakini hayapo sehemu nyingi, yaani yapo tu kama hizi Halmashauri za mijini, wilaya za mijini lakini huko ukiangalia hizi za pembezoni kabisa haya Mabaraza ya Ardhi hayapo. Vile vile haya Mabaraza ya Ardhi, napenda kwamba waajiriwe wataalam hasa wa kuweza kuishauri Serikali na vile vile waangalie utaratibu mpya kwamba je, tunawezaje kuisimamia hiyo Serikali katika sekta ya ardhi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nisemee fidia. Kwa kweli Mheshimiwa Waziri, fidia ni tatizo kubwa hasa katika Jiji la Dar es Salaam, fidia ni tatizo kubwa mno hasa tukiangalia katika miradi ya EPZ. Miradi ya EPZ unakuta uthamini umefanyika miaka 10 iliyopita, lakini mpaka leo wale wananchi bado bado hawajalipwa na zile nyumba zao wamepigwa stop order kila kitu. Sasa mnavyosema kwamba maeneo ya viwanda lazima yawepo, watafanyaje hiyo kazi ya kuweka miradi ya EPZ bila kumlipa mtu fidia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri yaani afanye hiyo survey kubwa kwenye hawa watu ambao hawajalipwa fidia, kwa sababu sheria inasema kwamba fidia iwe full, fair and prompt lakini hiyo haifuatiliwi kabisa. Ndani ya miezi sita iwe imeshalipwa, lakini hamna mtu anayefuatilia na mgogoro mkubwa unakuwa kwenye hilo tatizo la fidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisemee pia juu ya land rent intention, Mheshimiwa Waziri tukichukua kwa mfano Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam, Wizara wanapeleka tu ile 30 percent kama uwakala wa wale wanaokusanya lakini hawapeleki yaani 30 percent ya viwanja vyote kwa mfano wale walipa kodi wakubwa wanalipia Wizara ya Ardhi, hawaji kabisa kwenye Halmashauri. Sasa wanaporudisha ile 30 percent wanarudisha zile za uwakala tu ambazo Halmashauri wamekusanya, hawarudishi zile zote ambazo zinazostahili, kwa mfano, Halmashauri ya Kinondoni wairudishie majengo yote na viwanja vyote kwamba land rent yenu ni hii hapa mnayotakiwa kupata, sio tu waseme kwamba zile za uwakala tu ndiyo warudishe. Temeke wafanye hivyo hivyo na Ilala wafanye hivyo hivyo kwenye viwanja vyote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu vile vile niombe Mheshimiwa Waziri akija kuhitimisha atupe zile takwimu kwamba je, maana yake kwenye ukurasa wa 11 kwenye hotuba yake alisema kwamba bilioni nne amezirudisha kama land rent intention kwenye Halmashauri. Naomba atupe takwimu kwa sababu, najua kabisa yaani hizo asilimia kubwa hazirudi kama inavyostahili. Inawezekana kuna upungufu fulani wa hizi taarifa. Kwa hiyo, naomba akija kuhitimisha atuletee hizo takwimu alizokuwa amepeleka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile niongelee land bank. Mheshimiwa Waziri hawezi kufanya kazi bila kutenga maeneo wezeshi, lazimaauwe na maeneo ya ardhi hifadhi ambayo hata kama akija mwekezaji wasiende kumgombanisha kwa kumwambia tu nenda kule kijijini utaikuta ardhi au Wizara yenyewe inatoa tu mamlaka kwamba shamba hili hapa. Vile vile wamewapa mamlaka wale wanakijiji halafu vile vile wanaenda wanampeleka mwekezaji, hiyo migongano inatokea kutokana na kutokuwa na hiyo land bank, lakini ukiwa na land bank kama Wizara wanasema kabisa nenda sehemu fulani kawekeze hivi na hivi na wanampa hatimiliki wakisimamiwa na hiyo TIC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile naomba niongelee mradi wa Kigamboni City. Kwa kweli ule mradi ni tatizo na unaweza ukawa ni jipu!
MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.
MWENYEKITI: Ahsante.