Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya ya kupata nguvu ya kutoa mchango wangu katika Wizara hii muhimu ya Nishati na Madini. Pia, nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais Dokta John Pombe Joseph Magufuli, kwa hekima kubwa ya kumteua Profesa Muhongo katika nafasi ya Uwaziri wa Wizara hii. Ni kweli ametundendea haki Watanzania kwa maana upele umempata mwenye kucha katika Wizara ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Profesa Muhongo, Naibu wake, Katibu Mkuu wa Wizara na Timu nzima ya Wataalam Wizarani kwa mipango yao na mwanzo mzuri wa utendaji katika Wizara hasa kuleta umeme wa uhakika kwa sisi wa vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuishauri Serikali kuhusu leseni kwa makampuni ya uchimbaji wa madini; wakati wa kuitoa kwa wawekezaji hao (leseni) ni vizuri kuwashirikisha wananchi wa eneo husika kupitia viongozi wao, kwa maana ya wawakilishi katika vijiji, kata, jimbo na wilaya, ili kuondoa migogoro ya wananchi na wawekezaji katika meneo yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni vema ifahamike faida na manufaa ya uchimbaji huo kwa jamii na Taifa kwa ujumla, badala ya hali ya sasa mwekezaji anapata leseni Dar-es-Salaam na akifika maeneo husika halipi fidia wala service levies katika Halmashauri husika kwa kisingizio cha madini sio mali ya mtu na wao wameshalipia Serikalini kwa wamiliki wa madini hayo. Nashauri, kabla ya kutoa leseni, Wizara ni vizuri kufanya utafiti katika maeneo husika, ili kufahamu hali halisi ya eneo hilo la uchimbaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, machimbo ya marble katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, katika Halmashauri ya Morogoro, katika Vijiji vya Kivuma, Kata ya Kibuko, Tarafa ya Mkuyuni na Kijiji cha Masiyu, Kata ya Gwata. Wawekezaji hawajalipa fidia kwa wananchi na pia, kutolipia ushuru wa huduma katika halmashauri kwa miaka zaidi ya ya sita tangu waanze uchimbaji, Kampuni ya Zhong Fa!
Mheshimiwa Naibu Spika,Sababu hii imekosesha mapato stahiki kwa Serikali, kwa sababu mrabaha wanalipa katika mkoa uliosajili TIN zao, ambao uko mbali na machimbo husika, ambao hawajui kiasi halisi kinachopatikana. Nashauri katika suala la mrabaha washirikishwe TRA Wilaya na Mkoa husika wenye machimbo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, naomba kupatiwa umeme katika Kata ya Mkulazi vijiji vinne, Kata ya Mafuli vijiji vinne, Kata ya Kidugalo vijiji saba, Kata ya Ngerengere vijiji viwili, Kata ya Kiloka kijiji kimoja, Kata ya Gwata vijiji viwili, Kata ya Mkambarani vijiji viwili, Kata ya Mkuyuni vijiji viwili, Kata ya Kinole vijiji vinne, Kata ya Tegetero vijiji vinne na Kata ya Kibuko vijiji vyote vinne.
Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya vijiji 64 ni vijiji 16 tu ndivyo vyenye umeme, naomba katika REA III tupatiwe umeme katika vijiji hivi na kata hizi kwa ujumla, kwani hata huko tunakotaka kwenda katika uchumi wa viwanda, hasa Kata ya Mkulazi kwenye mradi mkubwa flagship wa Mkulazi Village afya na Bwawa la Kidunda ambalo vijiji vyake vina umbali zaidi ya kilometa 50 toka kijiji kimoja kwenda kingine; mfano Usungwa, Mkulazi, Usangara mpaka Kidunda. Naomba tupatiwe umeme ili katika REA nasi tufanane na Watanzania wenzetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.