Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara hii kama ifuatavyo:-
Nampongeza Mheshimiwa Waziri, Profesa Muhongo kwa hotuba yake nzuri iliyosheheni mambo muhimu kuhusiana na nishati na madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza kwa kupewa/kutengewa bajeti kubwa kwa lengo la kuboresha mambo ya nishati ambayo ni muhimu sana katika kuipeleka nchi yetu kwenye uchumi wa kati. Naomba nimwombe Mheshimiwa Waziri kwamba, wajitahidi kuhakikisha mipango inakwenda kama ilivyopangwa kwa faida ya wananchi wote wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nimwombe Mheshimiwa Waziri yafuatayo katika Jimbo langu la Chilonwa:-
Umeme wa REA Phase II ulikuwa ufike hadi Kata ya Zajilwa, Kijiji cha Zajilwa, lakini haujafika, naomba sasa ufike.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba umeme katika REA Phase III uende pia, maeneo yafuatayo:-
Vijiji vya Gwandi Bwawani na Magungu vilivyo Kata ya Zajilwa; Vijiji vya Izava, Umoja, Segala, vilivyo Kata ya Segala; Vijiji vya Ikombo, Solou na Itiso vilivyo Kata ya Itiso; Vijiji vya Manyemba, Chiwondo, Igamba, Nayu, vilivyo Kata ya Dabalo; Vijiji vya Chitabuli, Mlimwa, vilivyo Kata ya Membe; Vijiji vya Bwawani na Chalinze B vilivyo Kata ya Manchali; Vijiji vya Mlebe, Msamalo, vilivyo Kata ya Msamalo; Vijiji vya Makoja, Butiama, Ikowa, vilivyo Kata ya Ikowa; Kijiji cha Humekwa, kilicho Kata ya Haneti na Kijiji cha Kawawa kilicho Kata ya Msanga.
Mheshimiwa Spika, nawasilisha.