Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutatua kero na changamoto nyingi zilizopo katika Sekta ya Nishati na Madini nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi hizo namwomba Mheshimiwa Waziri au nimkumbushe ahadi yake ya kuvipatia umeme vijiji vifuatavyo vilivyopo katika Jimbo la Mchinga ambavyo ni:-
Vijiji vya Dimba, Ruvu, Namtamba, Ruchemi, Michee, Kiware, Mputwa, Lihimilo, Namkongo Matapwa na Mnyangara. Mheshimiwa Waziri vijiji hivi ni miongoni mwa vijiji vilivyopo Jimboni ambavyo havijapata umeme kupitia mradi wa umeme vijijini REA. Nakumbuka hoja hii kwakuwa tayari tulishawahi kuzungumza na Mheshimiwa Waziri kuhusu suala hili la umeme mara kadhaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine ni kuhusu suala la madini, Mheshimiwa Waziri kwanza nimpongeze kwa juhudi zake mahsusi za kunisaidia juu ya suala la wanakijiji wenyewe kuunda vikundi ili waombe hati za wachimbaji wa madini gypsum na kupeleka sokoni kama vile katika kiwanda cha cement Dangote. Mheshimiwa Waziri pamoja na msaada wake huo kwangu bado kuna haja ya Wizara yake kufanya juhudi za maksudi kuhakikisha kuwa maeneo yote yaliyopo Jimboni yanayohusishwa na upatikanaji wa gesi, mafuta na madini yamepimwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na uvamizi mkubwa wa watu kutoka maeneo mbalimbali kuja kurubuni wapiga kura wangu kwa kununua maeneo yenye madini kwa kiasi kidogo cha fedha. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri Wizara yake ifanye mkakati maalum na kukutana na wananchi wa Jimbo hili ili kuhakikisha kuwa maeneo yote yanayotiliwa mashaka kuwa yamo madini yapimwe ili kuwaokoa wananchi kutokana na kasi kubwa ya watu kutoka mbali kuja kuchukua maeneo haya kwa kuwapa fedha kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia TANESCO ihakikishe zoezi la upatikanaji wa mita za LUKU na kuunganishiwa kwa umeme kwa wananchi ambao wapo vijijini, wameshakidhi vigezo vya kupatiwa umeme. Jimboni kwangu kuna kaya zaidi ya 200 ambazo zimekamilisha taratibu zote za kuingiza umeme lakini kumekuwa na delay kubwa kwa TANESCO Lindi kuwaingizia umeme wananchi hawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante.