Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuwateua Mheshimiwa Profesa Muhongo na Naibu wake Dkt. Kalemani, tuna imani nao na tunawaombea pia tutawapa ushirikiano. Pamoja na pongezi hizo pia tunawapongeza sana Viongozi Wakuu wa Wizara hii, Katibu Mkuu na Watendaji wote wanayoyafanya katika kutekeleza majukumu yao vizuri sana, hongereni sana na naunga mkono hotuba.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi nina mambo mawili ya kuomba:-
(i) Mradi wa umeme wa upepo Singida tafadhali tunaomba sana mradi huo uanze, tuna makampuni mengi yanayotaka kuwekeza huko na mengine yalishafanya tathmini ya fidia kwa wananchi na wananchi wanasubiri kulipwa fidia. Hii itasaidia sana kutuliza maswali.
(ii) Wachimbaji wadogo wa Sekerike, Hondo na Samsaru wanaomba wapatiwe umeme, pia kuna wawekezaji ambao ni ASHANTA wamezuia maeneo ambayo hawayafanyii kazi yoyote, hivyo inaleta mtafaruku sana kwa wachimbaji wadogo. Naomba Wizara iliangalie ili itende haki ya kuwapa wananchi walio tayari.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.