Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza Waziri, Naibu Waziri na timu nzima ya Wizara ya Nishati na Madini kwa kazi nzuri hasa ya usambazaji wa umeme Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza Serikali izingatie mipango ya umeme Vijijini (REA) ili itekeleze mipango mizuri ya kusambaza umeme ambao ni muhimu kwa uchumi wa viwanda. Naomba Serikali izingatie utekelezaji wa miradi ya Halmashauri ya Mbeya ambayo wananchi waliahidiwa na kusisitiza kuwa bajeti ya kusambaza umeme katika Vijiji vya Halmashauri ya Mbeya umetengewa shilingi bilioni 52.
Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Wizara na Serikali kwa michakato ya miradi mikubwa ya madini ikiwemo niobium ya milima ya Panda Hill.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa 62 hotuba inaonesha haya madini ya niobium yanapatikana Wilaya ya Songwe. Naomba isahihishwe kuwa haya madini ya niobium yanapatikana katika milima ya Panda Hill (Songwe) Wilaya ya Mbeya na siyo Wilaya ya Songwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na madini ya niobium, milima ya Panda Hill yamegunduliwa madini ya calcium ambayo yanatumika kutengeneza mbolea ya NPK. Naomba Serikali iweke mkakati wa haraka kufufua mradi huu na kuwanufaisha wananchi wa Wilaya ya Mbeya, kuongeza uchumi na pia uzalishaji wa mbolea za NPK hapa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kupongeza shirika la TANESCO kwa kazi nzuri licha ya changamoto mbalimbali. Napendekeza, Serikali ichukue hatua za makusudi kupunguza mzigo mkubwa wa madeni ya TANESCO hasa yale ya fedha za kigeni. Kuna uwezekano mkubwa wa restructuring ya hii mikopo iwe ya shilingi badala ya forex. Pia hatua za makusudi zichukuliwe, kuondokana na kununua umeme kwa fedha za kigeni, kutoka kwa wazabuni wa TANESCO - ikiwemo Songas.
Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza Serikali iweke kipaumbele cha umeme wa joto ardhi ambao gharama iko chini na upatikanaji wake ni wa uhakika na hauna madhara kwa mazingira. Serikali ihakikishe mradi wa joto ardhi wa ziwa ngozi uanze na kukamilika haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ichukue hatua za kuimarisha rasilimali watu katika shirika la TANESCO ili iendane na usambazaji wa REA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.