Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa katika mipango ya uanzaji wa miradi ya Mchuchuma wa makaa ya mawe na Liganga chuma. Wizara ya Nishati na Madini tarehe 19/4/2016 ilijibu kuwa fidia ya kulipa wananchi itafanywa mwezi Juni, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe fidia hii ilipaswa kulipwa mwezi Februari 2016. Wizara ya Viwanda na Biashara imetenga sh. 5,000,000,000 Liganga na kwa Mchuchuma sh. 5,000,000,000 kiasi kilichopangwa ni sh. 10,000,000,000 ambacho ni kidogo ukilinganisha na fidia ya sh. 14,000,000,000. Naomba maelezo pesa nyingine ambazo ni pungufu zitapatikanaje ili ziweze kulipwa katika kipindi kifupi kilichobaki cha Juni, 2016.