Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha kwa Waziri wa Nishati na Madini vijiji ambavyo havipo kabisa kwenye mpango wa umeme wa REA Jimbo la Mbozi. Vijiji hivi ni pamoja na:-
Ikonga, Maninga, Iporoto, Twinzi, Halambo, Shasya, Mbuga, Rungwa, Hamwelo, Insani, Itentula, Mboji, Iyenga, Nsega, Ileya, Igaya, Magamba, Mtunduru, Naulongo, Iwalanje, Nambala, Mbulu, Myovizi, Ivufula, Isenzanya na Manyara.
Mheshimiwa Naibu Spika, niaba ya wananchi wa Mbozi naomba Mheshimiwa Waziri awasaidie ili waingizwe katika REA phase III.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia makaa ya mawe yanayochimbwa Kijiji cha Magamba na Kampuni ya Wagamba Coal Company katika Jimbo la Mbozi kuna changamoto zinajitokeza. Kampuni hii haijawahi kulipa service levy katika Halmashauri ya Mbozi tangu uchimbaji wa makaa ya mawe uanzishwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kampuni hii iagizwe kulipa service levy katika Halmashauri ya Mbozi ili kuchochea maendeleo. Pia kampuni hii ielekezwe kutengeneza barabara ya kutoka Magamba-Isansa-Shiwinga-Mlowo katika Jimbo la Mbozi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.