Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SEIF H. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwasilisha maombi makuu mawili. Moja, ni kuomba Wizara kuweka msukumo wa malipo ya fidia kutoka TANESCO kwenda kwa wananchi wa Kata ya Simbo, Chabutwa na Mwisi kwani kwenye ziara ya Naibu Waziri Mheshimiwa Merdard Kalemani alikuja Jimboni na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Tabora aliahidi mbele yake kuwa pesa za fidia zipo na hivyo wanasubiri wamalize tathmini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo naomba Wizara ipeleke msukumo kwa Meneja wa TANESCO ili kuweza kuwalipa wananchi wa Kata hizo husika ili kuondoa misuguano isiyo ya lazima, hizi ni fedha ambazo walipaswa walipwe toka mwaka 2010 mpaka sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Wizara ya Ujenzi na Nishati na Madini, napenda kuwasilisha mawazo yangu juu ya kuongeza substation nyingine ndani ya Wilaya ya Igunga tofauti na ile iliyopo Wilaya ya Nzega katika Mji wa Nzega Ndogo toka pale Nzega Ndogo kwenda Choma ni karibu kilomita 30 na kutoka Choma kwenda Ziba kwenda Igunga ni kilomita 50, jumla umeme umesafiri kilomita 110 bila kuwa na substation. Naomba pale Ziba tuwe na substation, iunganishwe umeme/waya toka Nzega kwenda Ziba ili kupunguza kukatika kwa maana njia ya Nzega Ndogo kwenda Choma nguzo zinapita kwenye majumba hivyo tukipata substation Ziba na network tokea Nzega, Ziba itarahisisha kupunguza tatizo la umeme Wilayani Igunga.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni hayo tu nawasilisha.