Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuendeleza Sekta ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jumuiya ya Ulaya inatekeleza sera ya malighafi (mkakati wa malighafi) kwa lengo la kukabiliana na upungufu wa madini muhimu kwa maendeleo ya nchi za Ulaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mkakati huo wa malighafi wa jumuiya kuna madini zaidi ya 26 ambayo Jumuiya ya Ulaya imeyawekea mkakati wa kuyatafuta na kuyapata kwa gharama yoyote, mahali popote yalipo. Nashauri Wizara itambue uwepo wa mkakati huo na ijipange vizuri kuwezesha Tanzania kunufaika na madini yaliyo katika kundi hilo la madini muhimu kwa kuzingatia mtazamo wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mkakati huo wa Jumuiya ya Ulaya wa malighafi raw material strategy. Jumuiya ya Ulaya inaelekeza nia yake kusaidia Mataifa mbalimbali katika jitihada zake za kutafiti upatikanaji na madini mbalimbali na kuweka kumbukumbu za uwepo madini hayo hasa madini muhimu. Nashauri Serikali ijipange vizuri kunufaika na mpango huo wa Jumuiya ya Ulaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tunajipanga kuwa nchi ya viwanda pamoja na jitihada nzuri zinazofanyika kusambaza umeme vijijini kuna changamoto ya umeme unaosambazwa maeneno mbalimbali kuwa wa low voltage. Nashauri jitihada ziongezwe za kuwekeza miundombinu ya kuongeza nguvu za umeme na hivyo kuondokana na tatizo la umeme wa low voltage. Kwa kufanya hivyo, itasaidia sana kupatikana umeme wa uhakika utakaosaidia mapinduzi ya viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia kielelezo namba nne katika ukurasa wa 83, kiasi cha gesi asilia kilichogunduliwa nchini hadi Aprili, 2016 ni asilimia 1.9 iliyoendelezwa. Iinaonekana kama nchi tuna kazi kubwa ya kufanya hasa kuendeleza kuweka mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji na kuwahimiza kuendeleza visima vya gesi ambayo imeshagundulika. Kama nchi lazima tujiulize kwa nini inachukua muda mrefu kuendeleza visima vya gesi asilia na tunatakiwa kufanya nini kuendeleza kwa haraka visima vya gesi asilia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.