Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kwanza kabisa kuunga mkono hutuba ya Waziri wa Nishati na Madini asilimia mia moja. Nishati na Madini ni sekta muhimu sana katika kuchangia Pato la Taifa letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nishati ni kichocheo kikubwa katika kuleta mapinduzi na mageuzi ya uchumi kutoka uchumi duni na tegemezi na kuwa uchumi wa kisasa na wa kujitegemea.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mwenyezi Mungu ameijalia nchi yetu vyanzo vingi kama siyo vyote vya nishati kama vile maji, jua, upepo, makaa ya mawe, gesi, joto ardhi na hata nishati kutokana na madini ya Urani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na neema hii kubwa ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia katika nchi yetu, kinachotakiwa hapa hivi sasa ni kuwekeza zaidi katika nyanja za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali yetu kupitia Shirika la Usambazaji Umeme nchini TANESCO na kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetekeleza miradi mingi mikubwa na midogo mbalimbali nchini naipongeza sana Serikali na hasa baada ya kugunduliwa kwa kiasi kikubwa cha gesi hapa nchini kumepelekea kuzalishwa kwa umeme wa gesi katika miradi ya Kinyerezi I na II na kuondokana na utegemezi wa uzalishaji wa umeme na maji na mafuta mazito.Uzalishaji huu wa gesi nchini ni chachu ya kuzalisha umeme kwa wateja na hasa wale wa vijijini na wa kipato cha chini.
Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini kwa jitihada zake kupitia Shirika la Umeme nchini na Wakala wa Nishati Vijijini REA kwa utekelezaji wa miradi ya Electricity V na ile ya Wakala wa umeme Vijijini katika maeneo kadhaa ndani ya Wilaya ya Mbogwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Serikali maeneo yaliyopelekewa huduma; Mbogwe, Ngemo, Nanda, Ilolangula, Isebya, Ikobe, Ikuguigazi, Lulembela, Nyakapera, Bukandwe, Masumbwe, Iponya, Nhomolwa na Lugunga. Hata hivyo zipo Kata mbili za Nyasalo na Bungonzi bado hazijapatiwa huduma hii muhimu ya umeme na inayo matumani makubwa kwa Serikali kupitia mpango wake kabambe wa REA Phase III. Vijiji vyote na Kata zote zitapata huduma hii muhimu ya umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Madini nchini imekuwa na mchango mkubwa katika ukuzaji wa Pato la Taifa. Wilaya yetu ya Mbogwe wamejali kuwa na madini ya dhahabu na zipo leseni za utafiti muda mrefu. Hata hivyo, zipo changamoto nyingi katika eneo hili la leseni za utafiti hasa utafiti wenyewe kuchukua muda mrefu.
Kampuni ya Mabangu inayo leseni ya muda mrefu wa utafiti katika maeneo ya Kata za Nyakafura, Lugunganya na Bukandwe. Utafiti katika eneo la leseni ya Mabangu Resolute umechukua muda mrefu sana na kupelekea malalamiko yasiyokuwa ya lazima kutoka kwa wananchi hasa wenye nia ya kushiriki katika shughuli za uchimbaji mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, maombi yametolewa mara kwa mara kwa Wizara kuitaka Kampuni ya Mabangu na mshirika wake Resolute wafungue mgodi na wakishindwa kufungua mgodi ni vyema wakaliachia eneo hilo wakapewa wachimbaji wadogo wadogo. Tunaikumbusha Wizara kuitaka Mabangu na Resolute wafungue mgodi kwa maslahi ya Wilaya yetu ya Mbogwe. Nawasilisha.