Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuipongeza Serikali na hususani Wizara ya Nishati na Madini kwa kuja na mpango wa bajeti itakayowezesha Taifa letu kuwa na umeme wa uhakika. Sekta ya Nishati ni muhimu katika kutekeleza dhamira ya Taifa ya kujenga uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri juu ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini chini ya REA na TANESCO. Tofauti na mipango ya REA katika kusambaza umeme Mkoa wa Kagera una upekee wake kutokana na ujenzi wa nyumba za makazi sehemu za vijijini. Wananchi wa Kagera kila familia hujenga mbali na familia nyingine katika familia ambazo hazijabanana. Kaya moja inaweza kuwa mita 100 – 200 kati ya nyumba moja mpaka nyumba nyingine. Hali hii inapeleka mgao wa kilomita mbili na nusu kila kijiji waishio sehemu ndogo tu ya kijiji. Changamoto hii wananchi na viongozi tumeiwakilisha kwenye ngazi mbalimbali za REA, TANESCO na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukrani kwa kazi nzuri iliyofanyika niombe na kushauri yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na vijiji kuwa vikubwa sana na aina ya makazi, tathmini ifanyike na waongezewe wigo wa usambazaji. Usambazaji wa umeme kwenye Jimbo la Muleba Kaskazini utoe kipaumbele kwa Kijiji cha Kahumuko, Kata ya Katoke na Omurunazi, Kata ya Mushabego kutokana na uwepo wa mashine za kusukuma maji ambazo zinatumia diesel.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Nyakatanga, Kijiji cha Bihija hakikutajwa, kihusishwe. Kata ya Rutoro nashauri Kijiji cha Misambya kihusishwe na izingatiwe kuwa kijiji kimoja kimeandikwa mara mbili.
Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri pia Kata ya Bumbiile ni eneo kubwa sana, kwa hiyo solar min grid ziongezwe ili kufikia vijiji vingi hasa wananchi wakazi. Kata ya Boziba, Kisiwa maarufu kwa shughuli za uvuvi na biashara ya samaki kisiwa hiki kiongezewe solar min grid ya umeme wenye uwezo wa kuhimili shughuli za kibiashara kadri ya mahitaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.