Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Ushetu halikubahatika kujengewa miundombinu ya umeme. Tumepata vijiji viwili tu. Tunao uzalishaji mkubwa wa mazao ya kilimo na misitu na tunahitaji kuchakata mazao yetu ili tuinue uchumi wa wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tumehamia Makao Mapya ya Halmashari ya Ushetu ambayo yako katika Kata ya Nyamilangano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni yangu Mheshimiwa Waziri, tupelekewe umeme kwa haraka Makao Makuu ya Halmashauri yetu ya Ushetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, tujengewe miundombinu ya umeme kwenye vijiji vyote REA II ili tuweze kuchangia katika kukuza viwanda na uchumi wa nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, Mheshimiwa Waziri nakushukuru kwa ushirikiano wako na nia yako thabiti kutusaidia wana Ushetu. Naunga mkono hoja.