Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimwa Naibu Spika, awali ya yote nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo, Mbunge na Waziri wa Nishati na Madini pamoja na Naibu Waziri wake Dkt. Kalemani, Mbunge, kwa kazi kubwa mnayoifanya. Pia nawapongeza watumishi na wafanyakazi waliopo kwenye Kamati hii chini ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa shukrani za pekee kwa niaba ya wananchi wangu wa Jimbo la Nyasa na mimi mwenyewe kwa kufikisha umeme kwenye Makao Makuu ya Wilaya, Mbamba Bay/Kilosa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nilimwandikia Mheshimiwa Waziri kwenye barua yangu, kimsingi nafahamu jitihada zinazoendelea katika kufikisha umeme kwenye Vijiji vyote 82 vya Jimbo langu kupitia REA III kama ambavyo nilifahamishwa. Natarajia kupitia dhamira hiyo, uwezo wake Mheshimiwa Waziri na ahadi ya Chama cha Mapinduzi iliyonadiwa na Mheshimiwa Makamu wa Rais siku ya tarehe 8/9/2016 – Tingi, suala hilo litakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, line kuu ya umeme wa Kilowatt 33 Mbinga – Mbamba Bay inapita kwenye msitu lakini pia katika milima na mabonde makali kiasi wakati mwingine kusababisha short na hivyo kukosesha umeme Mbamba Bay.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri kwa kuwa mpango pia ni kuendelea kusambaza line hiyo katika vijiji vingine vya Ziwa Nyasa hadi Lituhi, ni vyema kutengeneza T-off eneo la Kihegere ili kuunganisha line hiyo na ile iliyoishia eneo la Kipape – Chemeni, kiasi cha kusaidia endapo umeme wa upande mmoja kukatika. Kipande hicho ni kama Kilometa 15 – 20 tu. Pia naomba kuweka transformer katika Kijiji cha Mkalole na Makunguru kabla ya kufika Mbamba Bay. Jimbo letu la Nyasa ni changa kimaendeleo naomba lisaidiwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, lakini siyo kwa umuhimu, napenda kuwashukuru na kuwapongeza REA kwa jitihada zao katika kutekeleza majukumu yao. Tunawaomba mwendelee kupokea simu zetu bila kuchoka. Natanguliza shukrani zangu za dhati.