Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kuchangia hotuba hii kwa kumshukuru Mungu kwa kunijalia kuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge hili lako Tukufu.
Pili, nachukua fursa hii kwa kuwapongeza wananchi wangu wa Jimbo la Tumbatu kwa kunichagua kwa kura nyingi kuwa Mbunge wa Bunge hili. Natambua imani kubwa waliyonayo kwangu na naahidi sitawaangusha.
Tatu, napenda kumpongea kwa dhati Mheshimiwa Rais, Dkt. Magufuli kwa kuonesha imani na uwezo mkubwa wa kuongoza nchi yetu. Aidha, napenda kumpongeza Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa pamoja na Baraza lake la Mawaziri kwa uimara wao katika kuongoza Wizara zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tozo la KUA katika Kisiwa cha Zanzibar. Kwanza napenda kutoa masikitiko yangu makubwa kuona kwamba katika hotuba yote ya Mheshimiwa Waziri Zanzibar haikutajwa hata kidogo pamoja na kwamba ni miongoni mwa wateja wakubwa wa TANESCO.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, namwomba Waziri anieleweshe, kwa nini Zanzibar inatozwa bei kubwa ukilinganisha na wateja wengine? Kwa mfano, KUA moja inatozwa sh. 16,550/= kwa Zanzibar lakini kwa wateja wengine KUA moja (KUA) inatozwa sh. 13,200/=.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Serikali kwa juhudi inayochukuwa katika kuwapelekea wananchi huduma hii katika vijiji vyao. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri haikuzungumza vijini na maeneo yaliyosambaziwa umeme. Naomba Mheshimiwa Waziri aoneshe maeneo hayo (locations) na kiwango cha usambazaji (Kms) uliofanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia hali ya ujenzi wa line hizo haioneshi kama zimejengwa kwa wataalam wa mambo ya umeme. Inaonekana kuwa hakuna design yoyote iliyofanyika kabla ya kujengwa line hizo. Ni vyema, Makandarasi kwa usimamizi wa TANESCO wakalazimishwa kuwa na design pamoja na profiles ya kazi hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kawaida lifetime ya nguzo za umeme huwa ni zaidi ya miaka 20 lakini nguzo ambazo zinatumika katika kazi hii hasa za REA hazioneshi umadhubuti halisi kwa kazi hii. Hivyo nakuomba Mheshimiwa Waziri anieleze lifetime ya nguzo hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.