Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri mbalimbali hapa nchini kuna mabonde yenye mchanga ambapo siku za awali (nyuma) umiliki huo ulikuwa chini ya vijiji husika na kuwezesha vijiji hivyo kupata mapato.
Hata hivyo, katika miaka ya hivi karibuni, Wizara ya Nishati na Madini imebadili utaratibu huo na kukabidhi mabonde hayo kwa mawakala mbalimbali ambao wamekuwa wakitoza tozo tofauti kwa kila eneo na wakati mwingine mawakala hawa hutoza tozo hizi katika barabara kuu kwa kuweka road blocks kwa kushirikiana na askari wa barabarani. Kwa kuwa utaratibu wa tozo hizo ni chanzo cha mapato ya Halmashauri za Vijiji na wameweka katika by laws zao; na kwa kuwa utaratibu huo mpya haujawashirikisha vijiji husika, je, Serikali haioni upo umuhimu wa kupitia upya utaratibu huu kwa manufaa ya Serikali za Vijiji hapa nchini?
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Karatu ni mji wa utalii kwa kuwa ni lango kuu la kuingilia Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro. Tukitambua mchango mkubwa wa sekta ya utalii katika nchi yetu lakini baadhi ya vijiji katika Wilaya ya Karatu havina umeme. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Buger, Gongali, Endamanghang, Kansay na baadhi ya vijiji katika Mji wa Karatu?
Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.