Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini kwa hotuba yake nzuri yenye kuleta matumaini makubwa kwa Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Kuna tatizo kubwa la umiliki wa maeneo yenye udongo unaoashiria kuwa na madini. Maeneo hayo yapo chini ya Serikali za Vijiji na Halmashauri. Hawa watu wanaopewa leseni za umiliki wa maeneo haya bila hata Serikali ya Kijiji wala Halmashauri kujua ni kutengeneza migogoro na wenye maeneo yao na kuiona Serikali yao haiwatendei haki.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri aniambie ni utaratibu upi unatumika wa utoaji wa leseni hizi za umiliki wa maeneo haya yenye udongo wa madini? Leseni zinazotolewa zinadumu kwa kipindi gani? Katika tozo zinazotozwa mwenye eneo lake anafaidikaje? Halmashauri husika inapata nini kutokana na uharibifu mkubwa unaofanyika?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri anipe majibu.