Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia hotuba hii kwa maandishi. Matatizo ya REA phase II katika Jimbo langu na nchi nzima ni umeme kutofika kwenye taasisi nyingi katika maeneo ambayo umeme umepita na transformer kuharibika kwa muda mfupi baada ya kufungwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni ombi la upatikanaji wa umeme wa REA phase III katika maeneo ya Kata ya Monduli Juu, Mfereji, Moita, Naalarami, Migungani, Majengo, Esilalei, Mswakini, Makuyuni na Lashaine.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lingine ni ubovu wa Sheria za Madini ambapo katika maeneo yenye mchanga na kokoto, watu wanaenda kukata leseni ya madini ofisi za madini bila kupitia vijijini. Kuna uharibifu wa mazingira unaosababishwa na uchimbaji wa kokoto katika Kata ya Nanja.