Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukarabati jengo la Ofisi ya Madini Tunduru. Tunapongeza na kuishukuru Serikali kwa ukarabati huu. Tunaomba jengo hili liwe chanzo cha uwepo wa wataalam na vifaa stahiki kwa uboreshaji wa sekta ya madini hasa wachimbaji wadogo katika Kata za Ngapa, Muhuwesi na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, uboreshaji huduma ya upatikanaji wa umeme Wilaya ya Tunduru. REA phase II, vijiji 33 vinaendelea kwa usambazaji. Tunaomba kasi ya mkandarasi iongezeke, yuko taratibu sana. REA phase III vijiji 52 nilivyowasilishwa Ofisi ya REA na TANESCO Mkoa wa Ruvuma, naomba vijiji hivi viwe miongoni mwa vijiji kipaumbele vipate umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujua transformer iliyopata matatizo ya kiufundi matengenezo yake yamefikia wapi? Naomba changamoto zilizojitokeza kuhusiana na transformer hiyo iliyopatikana kutoka TANESCO zitatuliwe ili miradi iliyopangwa kutumia transformer hiyo ikamilishwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tunduma iko kati ya Songea na Mtwara. Umeme wa njia kuu (national grid) kutokea mradi wa SIDA kupitia Makambako, Songea unaishia Namtumbo pia umeme wa gesi na kadhakika. Kwa njia kuu kutokea Mtwara bado hatujaona wazi mpango wa umeme huu kwenda Tunduru.Naomba Tunduru iingizwe katika mipango ya usambazaji wa umeme kupitia national grid. Wakati tunasubiri mpango wa national grid Tunduru ipatiwe/iongezewe generators (DGs) zenye uwezo na ufanisi. Pia kutengeneza zilizopo na/au kuongeza nyingine kutoka maeneo mengine au mpya.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunaendelea na mipango yote, tufikiriwe pia kutumia/kupatiwa umeme wa nishati mbadala kwa kadiri itakavyofaa kitaalam. Zikitumika njia za biogas au ile ya kutokana na mabaki ya mazao (biofuel), basi njia hizo zinufaishe vikundi vya wananchi hasa akinamama kwani Tunduru ni mashuhuri kwa uzalishaji mazao ya kilimo.