Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Jambo langu la kwanza kabisa, kwa dhati namshukuru Waziri wa Nishati na Madini. Namshukuru kwa kuonesha nia ya kushughulikia tatizo lililoko Katika Jimbo la Nzega la wachimbaji wadogo na chuo cha MRI.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe taarifa Mheshimiwa Waziri na naomba AG ampe nafasi ili aweze kusikia hili tatizo Mheshimiwa Waziri, kwamba agizo alilolitoa Mheshimiwa Waziri la kumtaka mchimbaji aliyeingia kinyume na utaratibu, aliyeingizwa na MRI katika eneo la Resolute na mwezi mmoja aliopewa, pamoja na Waziri kupeleka delegation kubwa akiwepo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara, Kamishna wa Madini, yule mtu mpaka leo anaendelea na uchimbaji ndani ya eneo la Mgodi wa Resolute. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niliongea na Naibu Waziri Kalemani na tulishauriana juu ya solution ya jambo hili. Nataka niitahadharishe Serikali, tension iliyoko katika eneo lile, ni tension kubwa. Kwa hiyo, nashauri Waziri awaagize wataalam wake, yule mtu atoke ndani ya lile eneo kwa sababu perception ya wananchi juu ya lile eneo siyo jambo zuri sana. Hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Mheshimiwa Waziri anafahamu, nami nashukuru amenipa commitment, miradi ya umeme iliyokuwa inafadhiliwa na MCC katika Jimbo la Nzega kwa maana ya mradi wa umeme wa kutoa umeme Nzega Mjini kuupeleka Kitangili, kutoka Kitangili kwenda Migua; kutoka Migua kwenda katika Kata ya Mwanzoli, Kijiji cha Kitengwe. Naomba tuhakikishiwe wananchi wa Nzega kwamba mradi hii iliyokuwa inafadhiliwa na MCC itaingia kwenye REA Phase III, kwa sababu kuna upungufu mwingi katika miradi ya REA Phase II katika Jimbo la Nzega. Kwa hiyo, naomba Serikali itoe commitment katika jambo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka niseme katika hotuba ya Waziri, wazo la East African Countries kununua share kwa ajili ya kushiriki katika mchakato refinery kwenye project ya uzalishaji wa mafuta katika nchi ya Uganda, mradi huu ni jambo muhimu sana. Strategically ni muhimu kwa sababu maisha ya Watanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki, gharama za mafuta zitashuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Muhongo ni jambo la kuisukuma Serikali na sisi Wabunge tumsaidie ili Serikali ya Tanzania iweze ku-play part yake ili tuweze kupata shares zetu katika mradi huu na Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa sababu economically litatusaidia sana jambo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la mwisho, Waheshimiwa Wabunge, nimesoma hotuba ya ndugu yangu Mheshimiwa John Mnyika, kwa heshima Kabisa, tunajua suala la ESCROW mna hoja ya kumhusisha Waziri Muhongo, ni kutaka kumfanya kondoo wa kafara katika jambo hili. Naomba Bunge hili lisifanye makosa ya Mabunge yaliyopita kushughulika na watu dhaifu na kuacha msingi wa matatizo. We all know katika mioyo yetu suala la ESCROW kama beneficiaries wakubwa wa ESCROW wapo, wanajulikana. If we real want to deal with it, tuwafuate hao, lakini tumwache Mheshimiwa Profesa Muhongo atimize wajibu wake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ahsante.