Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. UKAWA naona mnashusha pumzi, kuweni na amani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende moja kwa moja kwenye hoja. Waheshimiwa Wabunge, Jimbo langu la Ulanga na Wilaya nzima imebarikiwa kuwa na madini ya kila aina kasoro tanzanite. Isipokuwa shida kubwa tunayoipata, wanasema mbega aliponzwa na uzuri wake, ndiyo shida kubwa tunayoipata Jimbo la Ulanga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Nishati na Madini, imejitenga kabisa na wananchi wa Tanzania. Wao wamekuwa madalali. Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini wanatembea na ramani za madini ya nchi hii makwapani, kazi yao kubwa ni kutafuta wawekezaji, wanawapa leseni, hawajali pale wanaishi watu; hawajali wale watu wanatakiwa wafidiwe na kama hata ni kufidiwa ni shilingi ngapi? (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, mtakubaliana na mimi, nendeni sehemu zote ambazo kuna uchimbaji mkubwa wa madini, watu wa pale wanaishi maisha duni sana, malalamiko makubwa sana yamejaa pale. Mheshimiwa Waziri nakuamini, Profesa maana yake ni mtu wa research, fanya research, haya yanatokana na nini? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeongea hivyo Mheshimiwa Muhongo, anajua namaanisha nini? Katika hotuba yake ame-specify kuna miradi mikubwa ya madini ambayo inatakiwa ianze; madini ya graphite ambayo katika Tanzania yako sehemu mbili; Ulanga na Ruangwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo wale wawekezaji waliowapa leseni wameshakuja kule wanataka kuwahamisha watu. Mheshimiwa Waziri ametuma watu wake waje kule waangalie: Je, kuna umuhimu wa wananchi kuhamishwa au lah? Wananchi wamelalamika, watu aliowatuma wamesema wamempa ripoti, wamesema watu hawatakiwi wahamishwe, Mheshimiwa Profesa Muhongo suala hilo limekwenda kwake, lakini bado ana kigugumizi. Kwa nini anashindwa kutoa kauli? Kuna nini katikati hapa? Wananchi wangu hawana amani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaambie, hii Wizara ya Nishati na Madini mwaka 2010 ilitoa hadi leseni ya Waziri mwenzao ilimpa mbia afanye uchimbaji wa madini kwenye nyumba ya Waziri mwenzao, Marehemu Mama Kombani. Hii Wizara ya Nishati na Madini iltoa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, ikampa mwekezaji achimbe madini; ilitoa Mahakama ya Wilaya; ilitoa eneo la wakazi zaidi ya 15,000, imempa mwekezaji achimbe; yaani hawajali, wanapotoa hawaangalii kama kuna watu wanaishi. Mheshimiwa Muhongo naomba alifanyie kazi. Wale wawekezaji aliowapa leseni, hawawezi kuchimba graphite, labda wakachimbe Jimboni kwake, lakini siyo Ulanga. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, napenda kuongelea suala la umeme. Umeme unazalishwa Kidatu tangu mwaka 1970. Kutoka Kidatu kwenda Ulanga ni kilomita 150. Imechukua miaka 20 Ulanga kupata umeme. Hata sasa hivi, umeme upo, kwa wiki unawaka mara moja. Mheshimiwa Profesa Muhongo, nilimwambia akatoe zile fito, aweke nguzo za kupitishia umeme. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu, Waheshimiwa Wabunge kuna jipu. Mheshimiwa Profesa Muhongo nimeshamwambia zaidi ya mara mbili, kuna hii sheria iliyopitishwa mwaka 2015 ya uagizaji mafuta kwa pamoja. Hiyo sheria inampa mamlaka Waziri ku-declare mafuta ya on transit yatumike nchini.
Hebu Waheshimiwa Wabunge fikirieni, imepaki meli pale ina mafuta lita laki tano; Waziri anaidhinisha yatumike nchini. Yale mafuta huwa hayalipiwi kodi, halafu sheria inampa nguvu Waziri kusema yeye ndio ataamua, yaani emergency condition ambazo yeye ata-declare. Sasa hiyo emergency condition hawajasema kuna sheria, yaani Waziri kichwani mwake siku hiyo kaamka kasema emergency condition leo ni hii, ana-declare. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Muhongo asisubiri aje aongee Mheshimiwa Zito hapa, asisubiri aje aongee Mheshimiwa Godless Lema, ni mimi Mlinga nafagia nyumbani, sawa! Naomba wakati anahitimisha aseme, la kwanza, kiasi gani cha mafuta ambacho amesha-declare cha on transit kitumike Tanzania? Kiasi gani cha kodi ambacho kimeshalipwa na ni lini analeta sheria hii tuifanyie marekebisho; hatuwezi tukamwamini. Dhamana yetu hatuwezi tukampa yeye. Mheshimiwa Profesa Muhongo, mimi leo sina mengi, ni hayo tu yanamtosha.