Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Unapotazama bajeti hii lazima takuwa-impressed na takwimu hasa kwenye kipato ambacho nchi hii inapata. Lakini utakuwa unajiuliza kama mwananchi kwa sababu utakuwa na matumaini kwamba tunaweza kutoka kwa mali ambayo tunayo katika nchi hii, mbali ya mali nyingine za misitu na bahari na kitu gani. Picha ya utajiri tulionao katika nchi kwa upande wa madini haionekani katika picha kubwa ya Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unaamini kwamba madini yangeweza kututoa kwa sababu wako watu wana madini au wana resource moja, mbili na wametoka na nchi zao zimekwenda mbele sana. Sasa sisi kama nchi ukitazama katika kitabu hiki unaona kuna mapato mengi, lakini unaweza ukajiuliza is this our level best, have we done our best katika suala la madini au la gesi? Kwa sababu siyo tu kuna room to improve, lakini naona kama kwamba unajiuliza, tatizo ni nini? Ni sera, ni mipango, ni utekelezaji, ni kitu gani? Kwa sababu zipo nchi ambazo zimeweza kutoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Angola ilikuwa na vita kwa muda mrefu, lakini baaa ya kutoka kwenye vita wamejipanga, sasa hivi wana kipato kizuri kinachopita dola 8,000 kwa kila mtu. Botswana nchi ndogo, ina GDP ya 38 au 39 billion dollars. Sasa hivi Mbotswana anapata dola 18,000 per capita yake na resource yao ni chache, uranium kubwa kabisa na vitu vingine vidogo vidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sisi Tanzania tunayo madini ambayo mtu mwingine katika Nchi nyingine angeweza kujiuliza why are you poor? Tusifananishwe na nchi kama Congo ambayo inautajiri mkubwa. Lakini Congo wana tatizo moja kubwa katika suala la utawala bora, lakini sisi tuna utulivu wa kutosha. Kwa hiyo, pamoja na uzuri wa kitabu hiki lakini ukisoma vitabu vingine viwili vya Hotuba ya Kamati na Hotuba ya Upinzani unaona kwamba kumbe tuna mengi ya kufanya ili tuweze ku-realise utajiri ambao Mungu ametujaalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na Mungu ametujaalia utajiri ule, ameuleta kwa sequence. Kila baada ya muda tunavumbua kitu kingine ambacho ni kizuri zaidi kuliko kitu kingine. Tulikuwa na almasi tangu miaka ya boers, imeondoka almasi ikaingia dhahabu sasa hivi Mungu katujaalia kuna madini makubwa zaidi ya graphite, tuna uranium inakuja lakini tunajipangaje katika hivi? Sasa mimi najiuliza, kwa mfano, tuna uranium na graphite ambayo ni madini very strategic, lakini je, tunayo sisi wenyewe strategic mineral policy?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyojua madini yanatumika yanakwisha lakini tunajipangaje madini haya yawe ya kututoa. Je, tunatengeneza sovereign fund kutokana na madini haya? Madini yatakwisha lakini nchi itabakia. Nchi inajitayarisha kwa mfuko ule ambao utaweza kuwa akiba kwa siku za mbele?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Qatar kweli ina gesi, Angola kweli ina petroli na vitu vingine lakini wana sovereign fund ambayo wanaweka akiba kwa ajili ya baadae. Sasa utajiri wote ambao tunao hivi sasa tunaojivunia, hatutawekea vizazi vyetu huko mbele lakini pia hatutoweza kufanya uwekezaji wa uhakika kwasababu kama nchi hatuna mfuko wa sovereign fund. Jambo hilo nimelisema hapa kabla na ninalisema tena kwa sababu mtu yeyote anaye study Qatar, Norway na wengine wamefaidika katika hilo. Sasa nilisema ukisoma hotuba ya Waziri, soma na vitu vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, twende kwenye REA. REA tunasema fedha zake zinajulikana zinapatikana njia gani na zimetengewa sheria kwamba lazima zitumike kwa njia ile. Jana tumeambiwa hapa kwamba shilingi bilioni 73 hazikutumika inavyopaswa. Unajiuliza kama shilingi bilioni 73 hizi zingetumika tungepata umeme kiasi gani kwa vijiji vyetu? Na kwa nini hazikutumika na zimekwenda wapi? Kama ambavyo wamesema watu wengine pia ningependa kumuuliza Bwana Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, makaa ya mawe ya Mchuchuma, Liganga kila mtu Tanzania amekuwa akiisikia. Kama nchi tuliwahi kujitayarisha kutumia sisi wenyewe ndani? Tumekuwa na mkakati wa kuongoza nchi kwamba hatuwezi kutumia makaa ya mawe? Makaa ya mawe haya kwa maana nyingine yapo lakini ni kama, kule Zanzibar wanasema kama joka la mdimu, yapo hayatusaidii kitu. Tumekaa nayo, hatuyauzi nje wala hatutumii hapa ndani kwetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni madini. Kama nilivyosema pale mwanzo, tuna madini ya kutosha, kumekuwa na malalamiko mengi hapa. Hata ile alama ya Tanzania (Tanzanite) bado hatuitumii inavyopaswa. Lakini mbali ya hayo, madini mengine mengi ambayo tunayo katika nchi yetu, hatujayatumia kiasi cha kutosha. Mimi naamini kama tungekuwa tumejipanga basi haya yangeweza kututoa. Tumeambiwa katika report ya Kamati kwamba kipato kwenye madini kimeshuka kwa asilimia 19, unajiuliza kitashukaje kwa sababu madini bado yapo kama kuna mikakati mizuri na mipango mizuri ya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahivyo mimi naamini tungefanya kazi vizuri katika eneo hili. Eneo lingine kama nilivyosema pale mwanzo, ni uranium na graphite. Tanzania, watu wengine wamesema hapa tunaweza kuwa katika kumi bora wa matumizi ya graphite. Graphite imekuja kama akiba yetu, kama hamadi kibindoni ambayo tunaweza tukaitumia ili nchi tuweze kusimama sawa sawa. Lakini kama nilivyosema mwanzo kama hatujakuwa na strategic mineral policy ambayo itatuongoza namna ya kuzuia vitu vyetu hivi basi hatutafika mbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine, jana nilisikia wazo ambalo nililipenda kidogo, wazo la STAMICO. Tunawekeza sana katika STAMICO, na dada mmoja hapa amesema, sehemu nyingine walizonazo STAMICO ziruhusiwe kwa wachimbaji wadogo wadogo; lakini lilikuja wazo zuri hapa. Wazo lenyewe ni kwamba badala ya STAMICO kung‟ang‟ania kuwekeza na kushindana na makampuni makubwa, kwa nini tusibadilishe format, STAMICO ikawa inanunua shares ambazo zitakuwa zina uhakika, kwa hili wazo ililtolewa na upande wa upinzani ambazo zitaweza ku-maintain hii kuliko kung‟ang‟ania kitu ambacho STAMICO hiyo enzi na enzi haijatutoa popote pale na bado tuko pale pale tulipo. Wazo hilo nimelipenda na ningependa Waziri alifikirie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni kuhusiana na suala la gesi. Ni kweli kama nchi tunajipanga kwamba tunataka kutumia gesi ikifika mwaka 2023. Lakini tujue tunajipanga, tuna majirani zetu Mozambique nao wana gesi ambayo inaweza ku-equal na kile ambacho tumekipata hivi sasa. Kwa hiyo, tujue tutakuwa na ushindani wa karibu, tena maeneo ambayo yamekaribiana. Kwahivyo mtu anaweza akachagua kuja Tanzania au kwenda Mozambique kwa sababu kijiografia ni maeneo yako karibu na kwahivyo kama hatujajipanga sawa sawa hatutaweza kufaidika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningeshauri, suala la LNG lingetazamwa mapema na namna ambavyo tutafaidika kwa sababu watu wote waliopata gesi wametoka. Qatar, Norway na wengine wote lakini kwa ambavyo mara nyingi naona katika nchi yetu tunaweza kuwa na gesi lakini bado tutakuwa maskini kwa sababu umaskini wa Tanzania kwa sehemu kubwa ni umaskini wa kujitakia. Ndiyo maana nakubaliana na hoja ya Kamati ambao wamesema, Serikali iandae mpango mkakati wa usimamizi wa gesi asilia pamoja na kutafuta masoko mapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia ya ushindani, tujipange kwa muda mrefu. Gesi na vitu vingine vinaweza kututoa lakini kama sivyo tunaweza tukabakia hivi badala ya kuwa economically giant tukawa economically dwarfs.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.