Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kupata fursa hii kuweza kuchangia hoja hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina mambo mawili, jambo la kwanza ningependa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Profesa Muhongo. Nampongeza kwa kazi aliyoifanya yeye na Watalaam wake ambao waliwezesha kupata tender ya kutoa mafuta kutoka kule Lake Albert Uganda mpaka Tanga bandarini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza kwa dhati kabisa, najua ilikuwa ni kazi kubwa, lakini mwishowe tumeipata! Pia nataka kusema tu kwamba Mheshimiwa Waziri tumepata hiyo kazi tunataka kujua kwamba tutafaidika vipi na hili bomba ambalo litapita kwenye Wilaya yangu na litaishia kwenye bandari yetu ya Tanga. Nafikiria kwamba ni vizuri wakajipanga na Waziri wa Uchukuzi kuona namna gani ambavyo wataweza kupanua bandari ya Tanga. Kuweka vitu vya kisasa kwenye bandari ya Tanga, kuhakikisha kwamba mafuta hayo basi, tunaweza kuyakidhi na kuyahudumia jinsi inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ningefurahi sana kama Mheshimiwa Waziri angeitisha kikao ili tuone kwamba tutafaidika vipi, tu-sensitize na wananchi wetu tuweze kuona tunaweza kuongeza value gani kwenye hilo bomba na tunaweza kufaidika nini kwenye hilo bomba.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, pia napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kutokana na mradi wa REA. REA imetusaidia sana, REA imetusaidia kupata Majimbo haya na mpango huu ni mpango ambao unatakiwa uendelezwe hata kwenye Idara nyingine ambapo tutakuja kuchangia kwenye mada zinazofuata.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Jimbo langu nafikiri linaweza kuwa ni Jimbo moja kubwa kuliko Majimbo yote hapa! Jimbo langu lina Kata 37, Vijiji 135, Vitongoji karibu 550, lakini mgao ambao umefanyika kwa REA awamu ya kwanza na awamu ya pili, vijiji ambavyo nimepata katika Jimbo la Muheza ni vichache sana! Namwomba Mheshimiwa Waziri aangalie kwa dhati kabisa aone kwamba hii awamu ya tatu, Jimbo la Muheza linaweza kufaidika namna gani. Nafikiri hatujazidi hata asilimia 40 kwenye mgao ambao tumepata! Vijiji vingi kwenye kila Tarafa, Jimbo lina Tarafa nne na kila Tarafa ina matatizo, kuna vijiji ambavyo havijapata umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Waziri aangalie, akitilia maanani pia Hale power station tunatoa karibu megawatts inaweza kuwa 20, pia ukijumlisha na Pangani tunatoa karibu megawatts 60. Kuna vijiji ambavyo viko karibu na power stations hizo, lakini usiku wao wanaangalia umeme kwa mbali tu. Kuna Vijiji vya Makole, Mhamba, Kwafungo na Songa vyote hivyo vinaangalia umeme usiku kwa mbali. Ningeomba aangalie kabisa aone ataweza kutusaidiaje!
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu alipoteuliwa tu, ziara yake ya kwanza ilikuwa ni Hale na naamini aliweza kuwaona hao wanavijiji ingawaje Hale haiko kwenye Jimbo langu iko kwenye Jimbo la Korogwe. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri ningeshukuru na ningefurahi kama angeweza kuliangalia.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine sasa hivi Muheza tuna matatizo makubwa ya transformer, tunayo transformer ndogo na ambayo ni chakavu. Sasa Serikali inapata lawama kubwa sana ya umeme kuzimika zimika! Tungeomba Waziri atutafutie transformer kubwa, kwa sababu tunataka tufaidike na hilo bomba, tunataka tuifanye Muheza kiwe kituo cha matunda. Sasa kama hatutapata umeme wa uhakika ina maana kwamba hata hivyo viwanda ambavyo tunategemea kuvijenga Muheza vitakuwa ni matatizo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri tungeomba sana ajaribu kuliangalia suala hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu ni Mkandarasi, nilishawahi kumwambia Waziri kwamba Mkandarasi Sengerema ana kazi nyingi sana! Speed anayokwenda nayo ni ndogo sana! Sasa nafikiri ni muhimu akampunguzia kazi ili tuweze kupata Mkandarasi mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana!