Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii, pili namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia nafasi nikaongea kwenye Bunge hili kwa leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Naibu na Wizara nzima kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naongelea kuhusu umeme wa REA nampa pongezi Mheshimiwa Waziri pamoja na Wizara nzima kwa upande wa umeme wa REA, kwa sababu umeme wa REA kwa kweli umesambaa kwenye mikao mingi na kwenye vijiji vingi. Umeme wa REA kwanza nashukuru kwa sababu pale ninapokaa nyumbani nashukuru sana Nyakayanja Nyeishonzi tumeweza kupata umeme wa REA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya shukrani hizo Mheshimiwa Waziri nakuomba sana tena sana, Mkoa wa Morogoro umejaliwa sana kuwa na mito mingi, Mkoa wa Morogoro una vyanzo vya umeme ikiwepo Kihansi pamoja na Kidatu lakini Mheshimiwa Waziri bado kuna vijiji vingi ambavyo havina umeme. Kwa hiyo, Phase I ya REA imepita, Phase II bado inaendelea, Phase III naomba mwezi wa saba ukianza naomba uweze kutupatia umeme kwenye vijiji hivi ambavyo havijapata umeme kwenye Wilaya zote za Mkoa wa Morogoro, Gairo, Kilosa, Mvomero, Morogoro Vijijini, Kilombero pamoja na Mlimba, Ulanga, na Malinyi naomba uwape kipaumbele kwa sababu ndiyo wana vyanzo vikubwa vya umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna nishati mbadala, nimeona kuwa utaipa kipaumbele, naomba sana uzidi kuipa kipaumbele kwa nishati mbadala au jadidi, kwa mfano biogas. Biogas ni rahisi hasa kwa wafugaji, biogas ni kitu rahisi ambacho kila mmoja anaweza akatumia, ni initial costs ambazo ndiyo kazi. Kwa hiyo, biomass pia, umeme wa jua, umeme wa maji, nguvu za maji na upepo kwa mfano Singida pamoja na Makambako ambao tayari ilishaainisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana uviangalie na hasa kwa sababu ukichukulia kuwa kutokana na tabia nchi na uharibifu wa mazingira watu wameanza kukata miti na kutakuwa jangwa. Lakini kama tutatumia hivi vyanzo ambavyo ni rafiki kwa mazingira kwa hiyo watu wataacha kutumia mambo ya mkaa na wataweza kutumia hivi vyanzo vingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Waziri naomba aangalie kuhusu bei ya umeme. Najua amesema inateremka lakini naomba iweze kuteremka zaidi. Pia gesi za kutumia nyumbani na zenyewe ni nishati, bei iko juu, naomba pia iweze kuteremka kwa sababu ikizidi kuteremka wananchi wengi wataweza kutumia hiyo gesi na wataweza kuacha kuharibu mazingira kwa kuchoma mkaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee mapato hasa mimi naongelea kwa upande wa vituo vya mafuta. Nimefanya utafiti mdogo kuhusu vituo vya mafuta, vituo vya mafuta tumeweka mashine, zile unapoweka mafuta zinakata risiti. Nashukuru kuna zile ambazo zinafanya automatic hata ukiweka lita moja unapata risiti yako, lakini kuna vituo mbalimbali ambavyo hizo mashine hazifanyi kazi na hao wanaouza mafuta wanafanya makusudi wengine hawazitumii hizo mashine na wengine wanatumia vitabu ambavyo mapato yetu hatuyapati kwa urahisi na wengine watu hawajawa na utaratibu wa kuomba hizo risiti kwa hiyo tunazidi kupoteza mapato. Kwa hiyo, naomba elimu itolewe na ufuatiliaji uweze kufuatiwa kusudi tuweze kupata mapato ya kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi kwa Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa Profesa Muhongo ambaye nimeshampa hongera, naomba sana wakati pale unajumuisha ingawaje hujatupatia orodha ya vijiji ambavyo vitapatiwa umeme kwenye mikoa yote wakati wa Phase III inayokuja, mimi nakuomba sana uweze kutupatia hiyo orodha ya vijiji ili tuweze kufuatilia na kuona na kuwaambia watu wetu kuwa umeme unakuja kaeni tayari. Hiyo ni nguvu zote na jitihada zote za Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachimbaji wadogo wadogo, nilikuwa naongelea kuhusu wachimbaji wadogo wadogo. Nakushuru Mheshimiwa Waziri umesema kuwa umewatengea maeneo. Lakini kumbuka kuwa kila mkoa kwa wastani kuna wachimbaji wadogo wadogo, nilikuwa naleta ombi kwako Mheshimiwa Mwenyekiti kuwa Mheshimiwa Waziri aangalie hawa wachimbaji wadogo wadogo waweze kuwapatia elimu. Naelewa kila mkoa au kila kanda kuna ofisi ya madini, hawa maofisa madini wanaweza wakakaa na hawa wachimbaji wadogo wadogo wakaweza kuwapatia elimu na ninaomba na wenyewe waweze kupatiwa ruzuku pamoja waweze kununua vitendea kazi kwa sababu haya madini ukishika hovyo hovyo kwa mikono unaweza ukaungua mikono.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kwa upande wa Mkoa wangu wa Morogoro, Wilaya ya Ulanga ambayo ina madini ambayo hayo madini nashukuru nasikia wanakuja wawekezaji, lakini imeanza mgogoro na hawa wananchi wa Ulanga ambao wanachimba madini yao wanasikia kuwa hawa wawekezaji wataweza kuchukua maeneo yao na hawa wananchi wamekuwa na vitalu vyao vya muda mrefu na wengine ni kurithi.
Kwa hiyo, naomba sana kusudi kukataza hii migogoro isitokee na kuendelea tuweze kuwapa elimu na kuwatengea maeneo yao hao wananchi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA:Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nakushukuru sana.