Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE.DKT. DALALY P. KAFUMU: Mhehimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mungu kwa kupata nafasi hii kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu, na nakushukuru na wewe Mwenyekiti kwa kunipa nafasi. Lakini kama wenzangu walivyosema tuwapongeze Waziri na Naibu Waziri, pamoja na wataalam kwa kazi nzuri wanayofanya katika mazingira haya magumu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua wana changamoto nyingi sana, mimi nilikuwa mmoja wao wakati fulani, kwa hiyo najua changamoto walizonazo, wanahitaji kuhudumia wananchi, lakini pia wanahitaji kuhakikisha wawekezaji wanaendelea kuja katika nchi yetu. Mnatakiwa kukaa katikati, ukihamia upande mmoja unaweza kuharibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nitasema maneno machache ya kutoa ushauri tu kwamba ukiangalia ukurasa wa 62 wa hotubua ya Mheshimiwa Waziri, kipengele 136, naomba nisome, kinasema; “Pamoja na bei ya madini ya dhahabu na nikeli kushuka katika soko la dunia, Serikali imeendelea kuhamasisha uendelezaji wa miradi mikubwa ya madini,” mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Waziri kwa kusema haya maneno, lakini ningependa sasa haya maneno ya-reflect katika vitendo vya Serikali katika kuhamasisha uwekezaji mkubwa. Sasa hivi ukipita mitaani huko ukisikiliza wawekezaji na wachimbaji wadogo kuna kilio kwamba Serikali imegeuka kidogo. Zile juhudi tulizofanya kuanzia mwaka 1995 Awamu ya Tatu na ya Nne zinakwenda tofauti kidogo, kwa hiyo mimi ningependa niwashauri Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, hebu ongezeni juhudi za kuhamasisha wawekezaji waje tusipohamasisha hatutakuwa na migodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi utafutaji na ninyi ni mashahidi umepunga kweli na utafutaji unapopungua maana yake ni kwamba hatutakuwa na migodi siku za usoni, hii migodi ikifungwa basi. Napenda niseme kwamba Kamati ya Bomani ilitushauri tukatengeneza sera nzuri, tukatengeneza na sheria nzuri, tumekosea wapi sasa mpaka tuanze kurudi nyuma? Ukiwasikiliza wawekezaji wengine wanasema Tanzania ninyi mnataka kurudi kwenye ujamaa, ukisikiliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi nashauri Mheshimwia Waziri, hebu tutoke hapo tulipo, tutengeneze mikakati sasa ya kuhamasisha. Kwa mfano tulikuwa tunaenda sana kwenye mikutano hii ambayo wawekezajiwote duniani wanakusanyika, tunawaalika. Miaka miwili iliyopita hatujaenda na wale wawekezaji wanaona Tanzania haimo tena kwenye kazi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaombeni sana tujitahidi tuwahamasishe wawekezaji, wasikate tamaa, ninyi ni mashahidi leseni nyingi sasa hivi zimekaa idle kwa kweli, japokuwa tumetengeneza mfumo mzuri lakini hazifanyi kazi kwa sababu tumekosea wapi, wataalam wa nishati na madini toeni ushauri jamani kitu gani kimetokea? Mimi inaniuma sanamnapoona juhudi zile za Serikali ya Awamu ya Tatu na ya Nne zinakwenda nyuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia majirani zetu Mozambique hata Malawi walitangaza geophysical results zao mwaka jana, sasa hivi wawekezaji wanaenda kule kutafuta dhahabu hii hii ambayo imeteremka bei. Kwa hiyo, mimi naomba sana na sisi tutazame tena wapi tumejikwaa, tuamke, ni ushauri tu ambao kwa kweli utatusaidia kwenda mbele upande wa madini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine napenda niseme juu ya ushiriki wa watanzania, tunaishukuru Serikali kwa kuwasaidia wachimbaji wadogo kuwapa hii mitaji. Lakini hebu wasaidieni pia na katika kutafuta madini. Geological Survey of Tanzania moja ya kazi yake kwa sera ile tuliyotengeneza ni kuyaangalia hayo maeneo ya wachimbaji wadogo na kuyapa value kidogo ili waweze kufanya kazi zao vizuri. Lakini pia ni kuwasaidia katika environmental impact assessment ili waweze kuwa na tija katika uwekezaji wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa kulisema ni ushauri ambao hua natoa kila mwaka na sasa hivi natoa, mnaweza msinielewe sasa lakini baadaye mtanielewa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), ni wakala unaofanya kazi nzuri kama walivyosema, lakini unalipa Taifa hili gharama kubwa kwa sababu unafanya kazi zinazofanywa na taasisi zingine. Ngoja nitoe mfano, wanaangalia kampuni itaweza kulipa kodi, kazi ambayo inafanywa na TRA mnaweza mkasema ni audit, lakini kazi ni ile ile ukimuuliza mwekezaji anayekaguliwa na TMAA, mwekezaji anayekaguliwa na TRA anayekaguliwa na yule mkaguzi wa kisheria kazi wanazofanya ni zile zile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunafumia hela nyingi kufanya jambo moja, ukiangalia wanafanya kazi ya ukaguzi wa mazingira, NEMC anakwenda kufanya jambo lile lile. Wanafanya kazi ya kuangalia madini yanavyopelekwa nje, wametengeneza ma-desk pale kwenye viwanja vya ndege, kazi hii ilitakiwa kufanywa na Ofisi ya Kamishna wa Madini kwa Sheria ya Madini ya mwaka 2010. Mimi nasema skills na taaluma tuliyoijenga pale, hebu tuiweke mahali inapostahili, mimi ningependekeza na nimewahi kupendekeza kwamba hii kazi ifanywe na mtu mmoja sio watu wengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunaweza tukaifanya TMAA ikawa Idara ya TRA yenye Kamishna wake wa ukaguzi wa migodi na hizo skills zote tukamuachia TRA, itasaidia sana badala ya kufanya kazi mara mbili. Taarifa ninayoipata lazima iende TRA na kama amekosea mtu, TRA ndio anaechukua hatua, TRA akiacha inakuwaje? Kwa hiyo TMAA imewekwa hapo kufanya kazi za watu wengine ili watu wengine wachukue hizo information. Tunatumia fedha nyingi sana, kufanya jambo lile lile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri tena, sasa hivi naweza nisieleweke nasema lakini siku za usoni nadhani nitaeleweka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho kama nitapata muda, nataka nizungumzie mikataba ya madini. Mikataba ya madini watu wengi wanaisema tofauti, Sheria ya Madini…
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Ahsante sana.