Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunifikisha hapa salama salimini. Napenda kukushukuru wewe kwa kunipa fursa na mimi niweze kuchangia katika mada hii ya Nishati na Madini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza Waziri mwenye dhamana, ndugu yetu Mheshimiwa Muhongo na Naibu wake kwa kufanya kazi kubwa katika Wizara hii. Kweli nia yake ya kuzima kibatari katika nyumba zetu na kwa wananchi kwa ujumla inaonekana. (Makofi)
Pili, napenda kuipongeza Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kunipa umeme katika vijiji vyangu 18, kikiwemo Kibiti, Nyamisati, Mchukwi, Bungu, umeme unawaka. Kwa hiyo, sina budi kuipongeza Wizara hii kwa kazi nzuri inayoifanya kwa kuwatumikia wananchi wa Jimbo langu la Kibiti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, viko vijiji kadhaa ambavyo havina umeme katika Jimbo langu la Kibiti lakini uwekaji wa miundombinu unaendelea. Cha ajabu ni kwamba kasi hiyo haiendani na matakwa ya wananchi. Vijiji hivyo ambavyo wakandarasi wako site ni kama Nyamatanga, Lungungu, Lwaluke, Kikale, Mtunda na Muyuyu. Naomba sasa Waziri mwenye dhamana afike na kuona kwa nini wakandarasi hawa wanashindwa kukamilisha miradi hii kwa wakati. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni fidia katika mradi wa umeme wa Kinyerezi, watu 400, kwamba cha ajabu kuna baadhi ikiwemo Dar es Salaam fidia hizo wamelipwa lakini wananchi wangu wa Jimbo la Kibiti mpaka leo hawajalipwa. Ukiangalia tathmini imepita muda mrefu, je, sasa Waziri huyu mwenye dhamana akija kuwalipa wananchi fidia hii watalipwa kwa bei ile ile au kwa tathmini nyingine? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti lipo tatizo katika maeneo ya Delta....umeme. Eneo hili la Delta lina kata tano, vijiji 16, vitongoji 27 mpaka leo hakuna hata kitongoji kimoja kilichopata umeme. Naomba Mheshimiwa Profesa Muhongo atumie jitihada zake zote kuhakikisha vitongoji hivi vinapata umeme hata wa nguvu za jua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sina budi kumpongeza Rais wetu, Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi anayofanya na sisi Wandengereko wote tuna imani naye katika kuhakikisha kwamba ataleta maendeleo katika wananchi wangu wa Jimbo la Kibiti na kwa nchi nzima kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine niseme katika matumizi ya gesi majumbani. Haya matumizi ya gesi majumbani wananchi wapewe elimu fasaha ili kwamba sasa watumie gesi waachane na kukata miti, mkaa na kuni. Umeme ndiyo njia ambayo itachangia kutunza mazingira. Katika nishati hii ya gesi kwamba watolewe vikwazo ambavyo siyo vya lazima kwamba gesi ipatikane kwe bei nafuu na kila mmoja aweze kuitumia majumbani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Kibiti viko vijiji 40 ambavyo bado havijapata umeme. Naomba katika Phase III iangalie vijiji hivyo ikiwemo Inyamatanga, Lwaluke, Matima, Lungungu na Itawatambwe nayo iangaliwe na tuhakikishiwe tunapata umeme katika Phase III. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nawapongeza wananchi wangu wa Jimbo la Kibiti, na mimi nawaahidi kwamba sitawaangusha, nitawapa ushirikiano katika kuangalia tunaleta maendeleo katika Jimbo langu la Kibiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine niseme viko vijiji ambavyo mradi huu unaendelea, lakini bado ujenzi wake hauendi kwa kasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo lingine niliseme ambalo ni changamoto ya Shirika letu la umeme (TANESCO) katika Wilaya yetu ya Kibiti, ni kwamba yako matatizo mengi ikiwemo usafiri, posho za ziada na maslahi yao ya kazi na elimu za fidia. Tunafahamu kwamba miradi hii ya REA haina fidia na inakuwa vigumu wananchi wanapokosa elimu, wanapokwenda kukatiwa miti yao inaweza ikaleta migongano baina ya wananchi na mtendaji husika katika maeneo yale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niseme kwamba naunga mkono hoja kwa asilimia mia kwa mia kwamba sasa wananchi wanahitaji maendeleo.