Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami kuchangia jioni ya leo. Awali ya yote, napenda kuwashukuru Wabunge wa Chama cha Mapinduzi kwa kunichagua kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM. Nawaahidi kwamba nitaitumikia nafasi hii kwa maslahi yetu na maslahi ya chama chetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo nampongeza Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa bajeti nzuri kabisa ambayo imetafsiri ile dhana ya Mheshimiwa Rais ya kwenda kwenye Tanzania ya viwanda, Mheshimiwa Waziri Profesa Muhongo nakupongeza sana. Hao wanaokubeza, naamini kabisa ndani ya nafsi zao wanajua kwamba katika viongozi wenye dira wewe ni miongoni mwao. Naweza kudiriki kusema kwamba wewe sio wa Kitaifa, bali wewe ni wa Kimataifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze moja kwa moja, kwenye upande wa umeme. Tumeona jitihada za Mheshimiwa Waziri na wataalam wake katika kuipeleka Tanzania kuondokana na changamoto mbalimbali za umeme ambazo ilikuwa inakabiliwa nazo huko nyuma. Tumeona coverage ya umeme ilivyoongezeka, upungufu wa bei, ongezeko la install generation capacity, kwa hiyo, nawapongeza sana. Naamini bado tuna changamoto kubwa katika sekta hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kumshauri Waziri na Wizara na sekta husika kwamba kuna maeneo inabidi tuzidi kuyafanyia kazi ili kuhakikisha kwamba ile dhamira ya kuwa na umeme wa uhakika na wenye kutosheleza inafikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye mpango wetu wa miaka kumi hadi mwaka 2025 tunatarajia kuwa na umeme usiopungua megawatts 10,000 na sasa tupo kwenye megawatts 1461. Kwa hiyo, tunatakiwa kwa hesabu za haraka haraka, kwa wastani kila mwaka tuongeze install generation capacity isiyopungua megawatt 948.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema ukweli Megawatts hizi ni nyingi sana na kwa kuiachia TANESCO peke yake hawataweza. Ninachokusudia kusema ni kwamba kuna haja ya kufanya reform katika sekta yetu ya umeme. Tunajua TANESCO imekabiliwa na changamoto nyingi katika muda mrefu. (Makofi)
Kwanza, shirika letu hili la umeme kwa kipindi cha takriban miaka minne sasa limeshindwa kuzalisha faida, linaendeshwa kihasara, kwa hiyo, halina mtaji wa kwenda kuwekeza kwenye uzalishaji wa umeme wote ule. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, hata ukiangalia vitabu vyao vya mahesabu, pia wana-operate katika deficit working capital. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba kabisa wakati umefika kwenda kufanya reform ya sekta ya umeme nchini mwetu. Serikali ifungue milango, wawekezaji binafsi waingie katika uzalishaji na katika usambazaji wa huduma hii muhimu kwa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii itatufanya kwanza kupata ongezeko kubwa la umeme kwa sababu tutafungua mwanya kwa wazalishaji wengi kuingia, lakini tutapata nafasi ya mashirika haya ambayo yanafanya usambazaji wa umeme ku-compete na kushusha bei ya umeme; na yenyewe yata-compete kwasababu yatakuwa katika business oriented. Naamini kabisa yataendeshwa kibiashara na yatazalisha faida tofauti na sasa ambavyo TANESCO inavyoenda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wa East Africa wote walikuwa na matatizo kama ya kwetu, wenzetu Wakenya walikuwa na kama ya kwetu au kuzidi ya kwetu; Waganda hali kadhalika, lakini walifanya reform kubwa kabisa katika sekta hii muhimu ya umeme, lakini hatimaye leo mashirika yao yanazalisha faida, hayaendi kwa ruzuku na pia wanapata wasaa wa kuchangia pato kwa Serikali kama sehemu ya gawio la Serikali. Kinyume na hapa kwetu ambapo Shirika letu la TANESCO mara zote limekuwa kila mwaka likiendeshwa kwa ruzuku ya Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naamini kabisa Mheshimiwa Profesa nia hii unayo, dhamira unayo na uwezo unao. Kwa hiyo, ni wakati sasa wa kufanya reform kubwa ya kuhakikisha tunaenda katika uzalishaji ambao ile dhamira ya kufikia kwenye Tanzania yenye viwanda tunafikia. Kwa sababu bila kuwa na umeme wa kutosha na uhakika, suala la viwanda litabakia kwenye vitabu vyetu na mipango yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango huo, niende kwenye upande wa EWURA. Nimepitia kitabu cha bajeti, ukurasa wa 80 kuna jedwali lile la bei elekezi za EWURA za umeme. Katika jedwali lile kuna vitu nimebaini niweze kusema ni changamoto ambazo naomba Mheshimiwa Waziri uzifanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia upande wa tariffs hizi za bei ya mahitaji ya juu (demand charges); mteja ambaye yuko katika T3HV (high voltage) wanachajiwa shilingi 16,550 kama tozo lao la bei ya mahitaji ya juu, wakati logic hapa hawa waliokuwa kwenye transmission line, cost ya kuupeleka umeme kwenye transmission line ni ndogo compared na cost ya kuupeleka umeme kwenye T3MV na T2, lakini wamebebeshwa mzigo mkubwa ambao hata najiuliza EWURA walipoweka hii bei walikusudia nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia wateja waliokuwepo hapa ni watatu tu waliokuwepo kwenye T3HV. Kuna Shirika la Umeme la Zanzibar, Bulyankhulu na Twiga Cement. Kwa mfano, kwa upande wa Shirika la Umeme la Zanzibar, ni bulk purchaser ambao waliingia mikataba na TANESCO ya Purchase Power Agreement ambayo sasa baada ya kuja EWURA ile mikataba imekuwa haina nguvu tena. Huyu ni bulk purchaser ambaye mwenyewe anatarajia huu umeme auze kwa wateja wake wa kati na wadogo. Sasa kama tunam-charge katika bei hii tunatarajia yeye auze kwa shilingi ngapi? Kusema ukweli katika kipindi kirefu kumekuwa na mlundikano wa madeni ambayo ZECO inadaiwa na TANESCO. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huenda moja ya sababu ya madeni haya naweza kusema ni appropriate tariff ambayo ZECO imekuwa ikitozwa kama ambavyo tunavyoona katika mwongozo huu wa bei ambao EWURA wameutoa mwezi Aprili. Kwa sababu wao wanachukua umeme katika transmission level ambapo gharama za depreciation, gharama za maintenance katika level hiyo ukilinganisha na wanaochukua T3MV na T2 ni ndogo lakini wamepewa…
MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.