Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi maalum ya barabara. Jimbo la Hai liko katika maporomoko ya Mlima Kilimanjaro, ardhi yake ni alluvial, ambayo huwa tope kali na zito lenye utelezi mkali na hatari hata kwa mvua kidogo sana. Barabara za lami hakika siyo anasa, hasa ukitia maanani hali ya miinuko na mabonde makubwa yaliyopo; barabara ya Kwa Sadala - Masama - Machame Junction ni muhimu sana sasa ikamilishwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara za mji wa Hai ambao ni makao makuu ya Wilaya nazo zinahitaji sana lami. Mji huu sasa unawakazi zaidi ya 60,000 na haujawahi kupata hata kilometa moja ya lami, ukiacha barabara kuu inayotoka Moshi kwenda Arusha inayopita katikati ya mji huu; tunaomba angalau kilometa kumi za lami katika mji huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Bomang‟ombe - Rundugai - Longoi - Kikavu Chini - TPC - Moshi, ni barabara muhimu iliyo ukanda wa tambarare. Ni eneo linalokumbwa na mafuriko mara kwa mara na miundombinu ya changarawe husombwa na hivyo kulazimika kujengwa kila mwaka. Barabara hii ina urefu wa kilometa 27, naomba sana iingizwe kwenye orodha ya barabara za kufanyiwa angalau upembuzi yakinifu kwa mwaka 2016/2017.