Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kuna ujenzi wa One Stop Inspection Station (OSIS) karibu utaanza eneo la Muhalala, Wilayani Manyoni. Ombi langu ni kulipwa fidia wananchi wa Muhalala ambao walitii kutofanya shughuli zote za kilimo na ujenzi eneo hilo wakisubiri fidia tangu mwaka 2013. Malalamiko ya wananchi hawa wazalendo ni makubwa, tafadhali nipate majibu, ni lini fidia hii inalipwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili; Manyoni Mashariki tuna barabara mbili za hadhi ya mkoa, kama vile Manyoni - Iteka - Sanza - Chali Igongo na Ikungi - Londoni - Kilimatinde (Solya). Tatizo langu ni kiwango cha ujenzi ni cha chini sana. Kiwango cha ujenzi hakitofautiani na barabara za Wilaya, wakati wa ujenzi hawamwagi maji ya kutosha, vifusi vinarashiwa sana, sehemu kubwa wanakwangua tu na graders, hawashindilii vya kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, culvets katika mapito ya maji ni vichekesho kwa baadhi ya maeneo, maji yanapita pembeni badala ya kupita ndani ya culvets. Upana wa barabara ni wa kuangalia upya, siyo rahisi kupishana mabasi au malori mawili yakiwa na mzigo kwani katikati pamenyanyuliwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja kubwa la mto mkubwa wa Sanza lililokamilika miaka miwili iliyopita limekatika. Kuna maajabu katika nchi hii, nashauri Waziri aidha, wewe mwenyewe au Afisa kutoka Wizarani nitampeleka akakague nondo zilizojengea daraja hili tulinganishe na BOQ, kuna hujuma mbaya sana. Tatizo kubwa ni usimamizi mbovu au wasimamizi Ofisi ya Meneja wa Mkoa wameungana na makandarasi kuwahujumu Wanamanyoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, reli ya Manyoni - Singida; tunaomba sana rejesheni huduma ya reli hii hata kama inashia Singida, ni sawa tu. Tuna vitunguu, viazi vitamu, kuku wa kienyeji, miwa, mbuzi, chumvi na mizigo mingine mizito kama mafuta kwenda na kutoka Singida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja.