Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Capt. Abbas Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Fuoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. KAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ununuzi wa ndege mpya kutoka Bombardier umefikia hatua gani? Ni lini hasa ndege hizo zitawasili tayari kwa kutumika (time frame)? Ndege ngapi zinategemea kununuliwa kwa hatua hii ya awali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Tanzania Airport Authority (TAA) mamlaka yake yanagusa pande zote mbili za Muungano (Unguja na Pemba)?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takribani miaka sita sasa cheo cha Ukurugenzi Mkuu wa Shirika la ATCL kimekuwa kikikaimiwa (acting), lini hasa utakuwa mwisho wa kukaimu? Je, unatambua kuwa ndege pekee inayomilikiwa na ATCL, Dash 8-300 imeacha kuruka toka tarehe 11/5/2016 na hakuna taarifa, kipi hasa kimesababisha hali hiyo? Naomba maelezo kuhusiana na hilo.