Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Naikumbusha Serikali suala la ujenzi wa bandari kavu ya Korogwe Mjini, eneo la Old Korogwe. Mheshimiwa Rais alipokuwa akiomba kura Korogwe, alikutana na hoja hii kutoka kwa wananchi na kuwaahidi atalifanyia kazi jambo hili, lakini kwenye vitabu vya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi hakuna mahali palipozungumzia suala hili la bandari kavu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Mheshimiwa Rais alitoa ahadi ya lami Korogwe Mjini, kilometa tano, lakini ndani ya makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti hii, Korogwe haijaguswa. Niiombe Wizara hii kuona ni namna gani itatekeleza ahadi hii ili wananchi waendelee kuwa na imani na Serikali yao. Naomba kuwasilisha.