Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mungu kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwa maandishi na pia kunipa uhai na afya njema ya kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kyerwa. Nichukue fursa hii kuipongeza Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, mwanzo ni mzuri, inatia moyo, ikiwemo Wizara ya Ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Murushaka – Murongo; Mheshimiwa Waziri katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi katika ukurasa wa 59 imeelezwa kufanyiwa upembuzi na usanifu yakinifu, lakini kwenye bajeti yako sijaiona. Mheshimiwa Waziri, kusema ukweli barabara hii ndiyo barabara ya kiuchumi namba moja Kyerwa, ndiyo tegemeo la Wanakyerwa ikipitia Makao Makuu ya Wilaya na kuunganisha Wilaya jirani ya Karagwe na kuunganisha Mkoa wa Kagera. Pia barabara hii inaunganisha nchi jirani za Uganda na Rwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri pia Mheshimiwa Rais akiwa Kata ya Nkwenda Wilayani Kyerwa aliitaja barabara hii na umuhimu wake na akaahidi itajengwa kwa kiwango cha lami na akatoa zawadi ya kuahidi kilometa 20 kwa kuanzia, wakati taratibu zingine zikiendelea, lakini cha ajabu ahadi ya kilometa hizo 20 haionekani katika Bajeti yako. Mheshimiwa Waziri, naomba kupewa jibu kwa nini hiyo barabara haipo kwenye upembuzi na hizo kilometa 20 alizoahidi kwa kuanzia, hazikuwekwa kwenye bajeti yako?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, kwa umuhimu wa barabara hii na mateso wanayoyapata wananchi isipowekwa kwenye bajeti au Mpango wa Serikali wa Miaka Mitano, tujiandae jimbo kuondoka. Maana wamekuwa wakiahidiwa maneno ya uongo kuwa itatengenezwa tangu Serikali ya Awamu ya Nne na Rais Kikwete akiwa Nkwenda kwenye mkutano wa hadhara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mgakorongo – Kigalama – Murongo; Mheshimiwa Waziri, naomba kujua barabara ya Mkagorongo – Kigalama mpaka Murongo, taarifa nilizozipata tayari imefanyiwa upembuzi yakinifu, ninachotaka kujua ni lini barabara hii ujenzi utaanza? Maana, sikuona kwenye bajeti yako pesa ya ujenzi kwa kiwango cha lami?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, nakuomba sana, nimejitahidi sana kukuandikia mpaka nimefika ofisini kwako kukueleza kuhusu barabara hizi na umuhimu wake. Naomba sana kufikiriwa, tumeachwa muda mrefu, tumekuwa yatima, hatukuwa na mtu wa kutusemea. Pia nikuombe sana, pata nafasi ufanye ziara ya kutembelea Jimbo la Kyerwa ili ujionee mwenyewe umuhimu wa barabara hii; maana inaonyesha wakati mwingine mnaletewa taarifa za uongo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipewe majibu kama nilivyooomba kwenye maandishi yangu. Naunga mkono hoja.