Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naunga mkono hoja, however, naomba majibu na utatuzi wa tija kwa haya yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ni tatizo hususani katika Mkoa wa Mbeya. Jiji la Mbeya kwa muda mrefu tumekuwa na kilio cha by pass road toka Mlima Nyoka, Uyole, barabara ya zamani kutokea uwanja wa ndege wa Songwe, tumejadiliana kwenye Road Board bila mafanikio. Kwani hii imekuwa ikisababisha foleni isiyopitika kwenye barabara kuu ya Mbeya, barabara kuharibika sana, ajali na vifo vingi kwani malori makubwa yamekuwa yakipita hapo hapo, hii ni hatari kubwa. Nahitaji jibu na ufafanuzi wa kina juu ya hili suala sugu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia suala la barabara ya Dar es Salaam, Tangi Bovu hadi Goba, huu ujenzi umesimama muda mrefu na eneo lililobakia ni dogo sana. Nini tatizo na lini itakamilika kwani itasaidia sana kupunguza foleni nyingine na hii barabara ni muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe unasuasua sana. Hakuna taa, jengo halijakamilika na ni gate way ya Southern Corridor; ni lini utakamilika kwa ajili ya kupanua wigo wa biashara hii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja wa ndege wa zamani wa Mbeya umekuwa dumped, umetelekezwa na hauna matumizi yoyote zaidi ya kuvamiwa hovyo, ni nini hatma ya uwanja huu? Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka kitega uchumi hapo au kuipatia Halmashauri ya Jiji, ili paendelezwe?
Mheshimiwa Mwenyekiti, cybercrime imekithiri, ni nini hatma ya hili suala? Mitandao imekuwa inachafua wananchi bila hatua yoyote. Tujulishwe udhibiti wake ukoje? Preventation ni better than cure, kuna wengine wanafahamika waziwazi; nipatiwe majibu ya kina na ufumbuzi kwa haya machache.Naunga mkono hoja.