Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi ya kuchangia japo kwa dakika moja kwenye Wizara hii. Kwanza nimshukuru kabisa Waziri wa Wizara hii kwa kazi kubwa wanayofanya. Pia nishukuru kwa daraja la Sibiti ambalo limetengewa pesa, tunaamini sasa litakamilika, ndoto hiyo itakuwa imemalizika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuna sera ya kuunganisha mikoa kwa mikoa kwa hiyo, barabara ya kuunganisha Singida na Simiyu bado hapa kupitia Iguguno, haikuweza kuonekana, kwa hiyo, nilikuwa naomba Waziri atakapojibu aweze kuzungumzia suala hili. Lakini katika ukurasa wa 252, kwenye Kasma 2326, kuna barabara ile ya kutoka Karatu - Mbulu - Haydom - Sibiti River – Lalago mpaka Maswa, hapo katikati inapita…
MWENYEKITI: Ahsante!