Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante. Ninaomba tu niende haraka haraka kwa sababu, muda nao ni mfupi sana, lakini pia nashukuru kwa nafasi niliyoipata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua suala la barabara ya Karatu - Mbulu limezungumzwa sana. Barabara hii ilimng‟oa Mheshimiwa Marmo baada ya miaka 25 kuwa Mbunge kwenye Bunge hili, kumbe ni kwa sababu tu mambo mengi kwa kweli hayapelekwi vile inavyokuwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa siyo hivyo tu, ilifika mahali wananchi wa Mbulu walikasirika wakaamua kuchagua debe la gunzi badala ya debe la mahindi mwaka 2010, lakini wamerudisha imani baada ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu, Makamu wa Rais, kupita wakati ule wa kampeni na yeye binafsi kupita katika barabara ile ya Magara akaona jinsi ambavyo anapita juu ya maji, alipofika daraja la Magara, akaahidi wananchi ya kwamba daraja hilo lazima litatengenezwa katika kipindi hiki. Tunamshukuru sana pia Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, kupitia kwa Waziri wake wa Ujenzi nina hakika ya kwamba, hili litakuwa limemgusa kwa namna ya pekee maana tumelisema sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa pili wa daraja la Magara kuna huduma muhimu kama shule na kituo cha afya, ambako wakati wa masika watu wa upande mwingine wa kutoka Mbulu hawapati huduma stahiki, wanafunzi wanashindwa kwenda shule wakati wa masika mpaka masika itakapokwisha. Tunaomba, haidhuru tujengewe daraja lile kama hatutaweza kupata barabara kwa kiwango cha lami ili kwamba wananchi hao waweze kuunganishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama hiyo haitoshi; daraja hili upembuzi yakinifu ulikwisha kukamilika na kwa namna hiyo kwa ajili ya ahadi ya Serikali ya tangu mwaka 2011 wakati wa Rais Mstaafu Kikwete, wadau mbalimbali kama TANAPA waliweza kusogeza huduma zao karibu. TANAPA wamefungua geti na REA tayari wamepeleka umeme pale wakijua kwamba daraja hili linatengenezwa karibuni ili wananchi wa pale wapate kuhudumiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme tena habari ya barabara ya Mbulu - Haydom. Haydom kama tulivyosema ni Hospitali ya Rufaa, ni hospitali kubwa inategemewa na mikoa kama minne, tunaomba tusaidiwe ili kwamba, wannchi wetu waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia ninaomba nizungumzie suala la FastJet. FastJet kwa kweli ni karaha, tunaambiwa kwamba hapa ni suala la soko, haiwezekani. Msafiri gani anasafiri bila begi?