Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naenda moja kwa moja kwenye hoja.
Naomba nimuunge mkono Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri, lakini nimwambie kwamba Barabara ya Tabora - Itigi - Manyoni kilometa 260, ambayo ameipangia shilingi bilioni 79 hizi za Serikali hazitatosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwepo Kuwait wakati tunazungumza na Kuwait Fund kuhusu kupata fedha kwa ajili ya barabara hii na walisema ikikamilika barabara ya Kilwa the next road itakuwa ni hii barabara ya Tabora - Itigi - Manyoni. Kwenye hotuba yake amegusia kidogo tu kuhusu hayo mazungumzo, lakini hajasema commitment ya Kuwait Fund ikoje, naomba wakati ana-windup atupatie commitment ya Kuwait Fund ikoje? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, barabara ya Makongorosi - Rungwa - Itigi hadi Mkiwa; hii barabara imeamuliwa kujengwa tangu miaka kumi iliyopita, ninaomba isifike miaka 20 barabara hii bado inajengwa, ninaomba sana. Hayo mawili yanamtosha Mheshimiwa Waziri kuyafuatilia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu cha tatu kiwanja cha ndege cha Tabora, amepanga pale shilingi bilioni 7.8; kiwanja cha ndege cha Tabora kilianza kujengwa mwaka 1919, hadhi yake ya sasa hivi iko nyuma sana ukilinganisha kwamba pale Tabora ndiyo makao makuu ya Western Brigade ya Jeshi. Ninaomba sana Serikali iweke kipaumbele kwenye kiwanja cha ndege cha Tabora; kwanza, hizo fedha shilingi bilioni 7.8 zilizopangwa zionekane kwa macho zimetumika, kusiwe na uchakachuaji wa aina yoyote Mheshimiwa Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu reli ya kati. Reli ya kati madhara yake ni makubwa sana kama haitajengwa. Kusafirisha mafuta kwa njia ya barabara petrol, diesel, mafuta ya taa, ni gharama kubwa sana na hii ndiyo inasababisha bei ya vitu hivi kuwa kubwa, inaathiri sana maisha ya watu wetu. Naomba sana kipaumbele, kwa njia yoyote ile Serikali ifanye lolote inaloweza kufanya hii reli ya kati lazima ijengwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo napenda kuchangia ni kuhusu bandari. Upo mradi unaoendelea pale, ule mradi unaoendelea wa kuboresha bandari kwa kushirikiana na Benki ya Dunia na Serikali ya Uingereza ninaomba usimamiwe vizuri, ili hatimaye meli kubwa ziweze ku-dock pale na ziweze kushusha shehena kubwa sana, ili tusiathirike kibiashara. Bandari yetu ina potential kubwa sana ya kusaidia uchumi wa nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo napenda kuzungumzia ni mitandao. Kwetu kule tuna shida ya mitandao kwenye kata nyingi sana, lakini hasa kwenye kata za Kilori, Kipili, Kitunda na Majojoro, ninaomba sana wakati Waziri anaposimama aweze kuzungumza commitment ya Serikali kuhusu kuboresha mitandao kwenye Wilaya yangu ya Sikonge. Ahsante sana.