Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Dakika tano ni chache, nianze tu kwa kusema kwamba Wilaya za Magu pamoja na Wilaya ya Ilemela inavyo visiwa, vinahitaji vipate vivuko kwa sababu visiwa hivyo ni vijiji. Katika Kisiwa cha Besi, Wilaya ya Ilemela, pamoja na Kisiwa cha Ijinga, Wilaya ya Magu, tumeomba kwenye RCC lakini mpaka leo na ninaangalia kwenye bajeti sioni, naomba Mheshimiwa Waziri aliweke hili ili tuweze kusaidiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo barabara ambayo imeahidiwa na Rais wa Awamu ya Nne na Rais wa Awamu ya Tano, barabara ya Ngudu - Magu pamoja Nhungumalwa kwa kiwango cha lami. Upembuzi yakinifu umeshakamilika, lakini nimepitia hotuba ya Mheshimiwa Waziri sijawahi kuona fedha za kutosheleza ujenzi huu wa mradi wa barabara ya lami. Naomba sasa aliweke ili ahadi ya Mheshimiwa Rais ikamilike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo Barabara ya Magu - Kabila - Mahaha; barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa Wilaya ya Magu pamoja na Bariadi. Mheshimiwa Rais ameahidi lami, lakini sijaona hata kwenye utaratibu wa upembuzi yakinifu, bali kuna hela kidogo tu ambazo zimetengwa kwa ajili ya kuendeleza barabara hii. Naomba barabara hii nayo ya Magu - Kabila - Mahaha, iwekwe kwenye mpango mzima wa lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo barabara inayofungua Mkoa wa Simiyu, kwa maana ya Bariadi - Salama - Sayaka - Bubinza na Kisamba. Barabara hii ni barabara ya karibu sana ikitengenezwa kwa kiwango cha lami ili kuepusha watu wa Bariadi kwenda mpaka Lamadi; ni barabara muhimu kiuchumi kama tunataka kujenga uchumi kwenye kanda hiyo. Tunaomba sana barabara hii iwekwe, lakini kipande hiki cha Sayaka - Bubinza - Kisamba, huwa tunaomba kwenye Road Board, kwa sababu ni kipande kidogo, kipande daraja kihudumiwe na TANROADS, lakini mpaka leo hakijaweza kuwekwa. Niombe Mheshimiwa Waziri akiweke kipande hiki, ili kiungane na wenzetu wa Simiyu na kiwekwe lami kipande hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, iko barabara ikijengwa tunaweza kuondoa msongamano wa Mwanza. Watu wa kutokea Mara wanapokwenda airport hawana sababu ya kuingia mjiniā€¦
MWENYEKITI: Ahsante! Ahsante,