Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha atueleze Tanzania ina Mabalozi wangapi na watumishi wangapi katika Bilozi zetu nchi za nje, lakini napenda utufamahishe ni Mabalozi wangapi kutoka Zanzibar na wangapi kutoka Tanzania Bara na hivyo hivyo kwa watumishi wa Balozi zetu zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kama kuna kasoro katika hili ulete utaratibu utakaotumia kuondoa kasoro ili isiwe kero ya Muungano.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia ulieleze Taifa ni kwa nini taasisi nyingi za Tanzania Bara ambazo sio za Muungano zinatumia jina la Tanzania hadi kufikia Zanzibar taasisi kama hizo kukosa uwakilishi wa kimataifa kwa kuambiwa tayari Tanzania ni mwanachama au vinginevyo, lakini Zanzibar inakuwa haina tena nafasi kwa mfano Tanzania Football Federation (TFF) ni mwanachama wa FIFA lakini Zanzibar imekataliwa sababu ya TFF.