Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipatia nafasi. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi hii na kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa najikita katika Sheria ya Mtandao iliyopitishwa na Bunge lako Tukufu mwaka jana. Naona hii sheria haijafahamika vizuri kwa wananchi, nilikuwa naomba Serikali iweze kufuatilia kwa undani zaidi utumiaji wa hii Sheria ya Mitandao. Je, ni lini Wizara yako itatoa elimu ili watu waielewe hii Sheria ya Mitandao, maana mitandao inatumika ndivyo sivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba pia kuhusu simu. Ni lini simu zitakuwa na rate moja? Kwa mfano, mtandao wa Vodacom au Airtel na Tigo kuwa na rate moja? Nilikuwa naomba pia Serikali iweze kulingalia hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mkongo wa Taifa umeenea nchi nzima, lakini internet inasumbua sana, baadhi ya maeneo ni shida. Unaweza uka-download kitu kwa muda wa masaa mawili, document. Labda una haraka sana ya kwenda sehemu unataka document uwasilishe sehemu, lakini inakuwa ni shida, nini maana ya kuweka Mkongo wa Taifa zima?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia network kwa vijijini imekuwa shida sana. Mtu unaenda vijijini unabeba simu tatu, atleast, upate communication. Unabeba labda simu ya Vodacom, Airtel na TTCL, hapo pote unatafuta communication. Nilikuwa naomba pia, hili iweze kuliangalia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, najikita moja kwa moja katika SUMATRA. Mara nyingi tunasikia SUMATRA ikidhibiti nauli za mabasi na treni, lakini kwenye nauli za ndege hakuna kudhibiti, ukiuliza unaambiwa inategemea soko kwa kuwa ni huria. Mbona basi ni huria na inazidhibitiwa? Unakuta ndege, kila ndege ina nauli yake, unakuta FastJet ina nauli yake, ATCL ina nauli yake, kila ndege ina nauli yake. Tulikuwa tunaomba na hili nalo muweze kuangalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa Kagera Airport. Kagera tuna Kagera Airport, lakini pia Ngara tuna uwanja wa ndege unaitwa Luganzo Airport. Huo uwanja wa Luganzo ulishasahaulika kabisa, hata hauongelewi katika Ilani ya CCM sijawahi kuona. Ule uwanja ulitumika sana kipindi cha wakimbizi, ndege zote za UN tulikuwa tunatumia pale. Na mimi ni mmoja wapo nilikuwa nafanya kazi UN, ndio tulikuwa tunatumia hata kuleta mizigo, cargo zote za wakimbizi zilikuwa zinatumia huo uwanja, lakini uwanja umesahaulika kabisa. Tunaomba Wizara hii iweze kuangalia ule uwanja wa Luganzo kama Serikali inaweza ikaanza kuutumia ili hata wawekezaji wa ndege waweze kutumia ule uwanja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, najikita pia katika ujenzi wa nyumba za watumishi wa umma. Watumishi wa umma wana tatizo la makazi kutokana na uhaba wa nyumba za Serikali. Unakuta mtumishi wa Serikali amehamishwa kutoka kituo kimoja kwenda kingine, anakaa hotelini muda mrefu sana, hapa hela za Serikali zinazidi kutumika. Kabla ya kuhamishwa kwa nini asitafutiwe nyumba ili Serikali kuweza kuangalia hizo hela zisiende bure. Nyumba hazina hadhi bora kwa…
MWENYEKITI: Ahsante.