Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa fursa hii. Awali ya yote naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Ujenzi lakini pia nimshukuru Mheshimiwa Waziri husika wa Wizara hii kwa mara ya kwanza ameweza kuona umuhimu wa Jimbo la Kilindi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka nianze kwa kuchangia hususani katika upande wa barabara kwenye dhana ya kuunganisha mikoa kwa mikoa kwa maana ya barabara kiwango cha lami. Nikienda ukurasa wa 41, hapa nataka nizungumzie barabara inayoanzia Handeni kwenda Kibirashi, Kijungu, Kibaya, Njoro, Chemba, Kwa Mtoro hadi Singida, ina urefu wa kilometa 460. Dhana hii ya kuunganisha mikoa ni dhana pana na ina maana kubwa sana kwa sababu inalenga katika uchumi wa mwananchi mmoja mmoja, Wilaya, Mkoa hadi Taifa. Unapofungua barabara maana yake unaruhusu mazao yauzwe kwa wepesi, unaruhusu movement za watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii katika mwaka wa fedha unaoanza 2016/2017 wametufikia katika stage ya visibility study na detailed design. Mimi nataka niamini kabisa kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa sababu inaunganisha mikoa minne, Mkoa wa Tanga, Mkoa wa Manyara, Singida pamoja na Dodoma. Muda umefika wa kuweza kuitengeneza barabara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine ambalo limezungumzwa na Wabunge wa Mkoa wa Tanga na mimi lazima nizungumze, hususani suala la reli ya Tanga kwenda Moshi hadi Musoma, na pia nataka nizungumzie habari ya bandari. Mambo yote haya ni ya msingi kwa sababu yanalenga kuinua uchumi wa Tanga. Waziri wa Viwanda alizungumza hapa kwamba kuna wawekezaji ambao wanataka kufungua viwanda katika Mkoa wa Tanga. Sasa kama unataka kufungua Mkoa wa Tanga maana yake nini, ni lazima uwe na bandari na reli iliyo imara ili uweze kusafirisha cement ile katika mikoa ya pembezoni mwa nchi. Mimi naomba Mheshimiwa Waziri hili ulitie mkazo mkubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo ningependa kuchangia kwa sababu muda hautoshi ni juu ya wakandarasi wetu ambao wanatengeneza barabara. Barabara nyingi hususani katika Halmashauri zinatengenezwa chini ya kiwango na wakati mwingine mkandarasi anatengeneza barabara haweki matoleo. Hili linasababisha barabara hizi kuharibika hasa wakati wa mvua. Mfano katika Jimbo langu la Kilindi lenye squire meter 6,125, Mheshimiwa Waziri nikuambie barabara hizi sasa hivi hazipitiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamenituma kwamba tuangalie ni namna gani mfuko huu wa TANROADS unaweza kusaidia kuikarabati barabara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine ni ushauri tu katika Wizara hii kwamba pawepo na performance audit katika miradi yetu mikubwa ya barabara. Miradi hii wakandarasi wanapewa hela nyingi sana, lakini baada ya mwaka mmoja, miezi sita barabara hazipitiki. Hii haiwezekani, Serikali lazima iwe very serious na hili, ili fedha za Watanzania ziwe na maana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala lingine ambalo ningependa kuchangia ni suala la mawasiliano…
MWENYEKITI: Ahsante.