Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amefanya leo nikapata nafasi hii. Lakini moja kwa moja niende kwenye mada. Kwanza nimpongeze sana Mkurugenzi Mkuu wa TANROADS, Engineer Patrick Mfugale, lakini pia nimpongeze sana na Meneja wetu wa TANROADS wa Mkoa kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie habari ya barabara zetu za Kilolo. Wilaya ya Kilolo iko katika Mkoa wa Iringa, ukienda kwenye Ilani ya Chama chetu cha Mapinduzi inasema kwamba kila barabara inayounganishwa na Wilaya itawekwa lami. Barabara zote ambazo zinakwenda Wilaya za Mufindi na Iringa zina lami. Juzi kwenye swali langu niliuliza miaka saba imeanza kushughulikiwa, kati ya kilometa 35 ni kilometa saba tu ndizo ambazo zimewekwa lami, kwa miaka saba kilometa saba ndizo zimewekwa lami. Nilikuwa nauliza tu swali na hata juzi niliuliza kwamba kwa kilometa hizi zilizobaki ambazo ni karibu 28, je, ni kwa miaka 28 ndipo tutapata lami? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeomba Mheshimiwa Profesa wewe ni mtu makini na kilolo unaijua, umeshafika, hebu angalia uwezekano wa kuhakikisha kwamba, barabara ya kutoka Ipogolo kwenda Ndiwili - Ihimbo - Luganga - Kilolo inawekwa lami; walau tupate kilometa saba tu kwa mwaka huu wa fedha na mwakani ukitupa saba basi tutakuwa tumesogea, ili watu wawe na imani. Kwa sababu ukiangalia katika Mkoa wa Iringa maeneo ambayo yanategemewa kwa kilimo ni pamoja na Wilaya ya Kilolo. Sasa tusiposafirisha yale mazao yakafika kwenye Wilaya nyingine na baadhi ya Mikoa ambayo ina matatizo itakuwa ni tatizo. Kwa hiyo, nakuomba kabisa uhakikishe kwamba angalau mwaka huu tunapata lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, nikushukuru kwa kuwa barabara hii ya Mkoa ilikuwa inashia Idete na juzi nilipokuwa nauliza swali langu na tulishaomba kwamba barabara hii kwa kuwa inakwenda kutokea Mkoa wa Morogoro kupitia Idete - Itonya - Muhanga mpaka Mngeta kwa Mheshimiwa Susan Kiwanga, ningeomba hizo kilometa 26 ambazo zimebaki pale, wala pale hatuhitaji lami tunahitaji tu pesa kidogo tuweze kuunganisha ili iwe rahisi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na nilisema kwamba leo hii ikitokea barabara ile pale Kitonga, aidha, pakaziba au pakabomoka uwezekano wa kwenda Morogoro unapotoka Zambia, Malawi, Afrika Kusini, Mbeya na Iringa yenyewe inabidi uje Dodoma, karibu zaidi ya kilometa 400 za ziada. Kwa hiyo, ningeomba Mheshimiwa kwa kuwa ulituahidi juzi hebu angalia uwezekano wa kutusaidia hizo kilometa 26 za kwenda kutokea Mngeta. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, ningependa kuzungumzia barabara nyingine ambayo inaanzia Ilula - Mlafu - Wotalisoli - Mkalanga - Kising‟a mpaka Kilolo, barabara hiyo ni ya Mkoa na ninashukuru Mungu kwamba imeanza kufanyiwa kazi. Ningeomba tu kwa kuwa barabara ile ni ya mkoa ina vipimo maalum ambavyo inabidi vizingatiwe. Na sisi Kilolo tumeweka msimamo kwamba tusingependa kwa wafanyakazi ambao hawatumii utaalam wakatoka nje ya mikoa yetu. Kama barabara ya Kilolo inatengenezwa basi vibarua watoke Kilolo badala ya kutoka maeneo mengine ili iwe rahisi wao kulinda zile barabara zao, kuona kama kuna udanganyifu kutoa taarifa kwa viongozi kwamba hapa tunaingizwa mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pi kuna madaraja pale. Nashukuru mmetaja habari ya madaraja kwamba mtatusaidia…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)