Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia kwenye bajeti hii ya mtoa hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ningependa kusema kwamba bajeti hii kwa kweli haikututendea haki Mkoa wa Tanga. Bajeti hii haiku-take into consideration kwamba sasa hivi tumepata tender, tumepata zabuni ya kutoa mafuta kutoka kule Ohima, Lake Albert - Uganda mpaka Tanga kwenye bandari ya Tanga. Lakini ukiangalia kitabu hichi hakizungumzi hata kidogo, hakuna hata mstari mmoja unaozungumzia kwamba Bandari ya Tanga itaboreshwa namna gani? Sasa hivi Bandari ya Tanga ina matatizo mengi, Bandari ya Tanga ina vitu ambavyo ni vichakavu, hata mashine za kubebea makontena ni taabu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hizi mashine za tag boats ambazo zinatakiwa kwenda kufunga meli baharini. Mashine ziko mbili, moja ni mbovu kabisa na nyingine tumekodisha kutoka Mombasa. Sasa sioni chochote ambacho kinaelezea mambo ya standard gauge kuhusiana na reli, sioni chochote ambacho kinaelezea kuhusiana na airport ya Tanga, mambo yote ambayo yanazungumzwa hapa ni standard gauge ya reli ya kati, au kwa sababu Waheshimiwa Wabunge wako kwenye mstari wa reli ya kati basi Tanga tunasahaulika? Kwa nini Tanga tunasahaulika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jana hapa Wabunge wa reli ya kati walikutana, sasa jamani Mheshimiwa Waziri nini sisi Tanga tumekukosea? Tumepata tender na hutaki kutupa chochote. Nimeona hapa maboresho ya Bandari ya Tanga ni shilingi milioni 7.6 kweli, are we serious? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nahamia sasa Jimboni kwangu kuna barabara kule, nimeangalia kwenye Hansard tangu mwaka 2000 barabara ya Amani - Muheza kilometa 40 imeanza kuzungumziwa, kwamba ijengwe kwa kiwango cha lami. Awamu ya Nne Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliahidi kuiweka barabara hiyo lami, Rais, Mheshimiwa Magufuli ameaihidi kuiweka lami barabara hiyo, Mheshimiwa Rais Mkapa ameiahidi kuiwekea lami barabara hiyo, na watu wote wa Amani wanategemea kwamba barabara hiyo itawekwa lami. Sasa hivi naangalia kwenye kitabu hapa naona shilingi milioni 250, nilitaka kuzirai Profesa, kwa sababu nitawaambia nini watu wa Amani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inategemewa kule, uchumi wa Muheza unategea Amani, mazao ambayo yako Amani ni kitukingine. Amani kuna kila kitu, kuna si mambo ya utalii tu, mbao, karafuu, chai, hiliki, pilipili manga na mdalasini zote zinatoka kule.
Sasa mimi nitawaambia nini watu wa Muheza jamani? Nategemea kwa kweli Mheshimiwa Waziri utakapo-wind up jioni basi ueleze chochote ambacho kitahusiana na barabara ya lami ya Amani, Bandari ya Tanga, reli standard gauge tunataka Tanga na kiwanja cha ndege cha Mkoa wa Tanga utakifanya nini. Sioni chochote wala hata kugusiwa hakikugusiwa; na sasa hivi tunategemea kwamba mambo yatakuwa moto moto Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeahidiwa kilometa tatu, Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli alifurahi wakati wa kampeni jinsi uwanja ulivyojaa, akasema Muheza mmenifurahisha nawapa kilometa tatu za lami vumbi limezidi, na hizo kilometa tatu mtazipata kabla ya mwezi wa sita; mpaka sasa hivi sioni kitu. Nimeangalia kwenye kitabu kuanzia page ya kwanza mpaka ya mwisho sioni chochote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri utakapokuja hapa kwa kweli utueleze na uwape matumaini watu wa Muheza hizo kilometa tatu za kuondoa vumbi Muheza utazifanya vipi, nitazipata namna gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala mengine niliwahi kuwasiliana Mheshimiwa Waziri, hakuna mawasiliano huko Amani ambako ndiko kwenye uchumi wetu Muheza. Hakuna mawasiliano Amani, Zirai, Kwezitu, Mbomole kote kule huwezi kuongea na simu, ukiongea na simu mpaka upande juu ya miti ama kwenye kichuguu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana nategemea kwamba Mheshimiwa Waziri labda atakuja na majibu, ahsante sana.