Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. William Mganga Ngeleja

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. WILLIAM M. NGELEJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa hiyo fursa uliyonipatia ya dakika tano, nashukuru sana. Nimesimama hapa kuungana na Waheshimiwa Wabunge wanzangu kuchangia hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambayo inatuunganisha Watanzania endapo mambo haya yatatekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaendelea kuchangia, wiki moja iliyopita Taifa zima lilipata habari ya mauaji yaliyotokea Jimboni Sengerema. Nasimama hapa kwa niaba ya Wanasengera na Watanzania wengine kuwaombea marehemu wetu waliouwawa kikatili sana, Mwenyezi Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia navishukuru sana vyombo vya habari kwa jinsi ambavyo vimezungumzia jambo hili na kupeleka ujumbe mahsusi kwa jamii. Kwa fursa hii navishukuru na kuvipongeza sana vyombo vya dola kwa namna ambavyo vimefanya kazi kubwa na kwa kweli sasa hivi watuhumiwa wameshatiwa mbaroni na naamini kwamba haki itatendeka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii kwa sababu ya matumaini kwamba yakitekelezeka yaliyomo humu ndani Taifa litakuwa linasonga mbele kwa kasi kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ninalotaka kuzungumzia ni masuala ya jimboni kwangu. Nimeona pale kuna masuala ya ujenzi wa daraja la Kigongo Busisi, zimetengwa shilingi milioni 600, naipongeza sana Serikali kwa ajili ya kupata Mhandisi Mshauri ili afanye usanifu, mambo ya design na mambo mengine ili hatimaye ujenzi wa daraja uanze, naishukuru sana Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mwaka jana tulipitisha bajeti ya ununuzi wa kivuko kingine hapo hapo Busisi Kigongo na hapa tumeelezwa kwamba taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu, taratibu za kufanya upembuzi yakinifu ulishakamilika na sasa taratibu za manunuzi ya hicho kivuko yanaendelea vizuri. Nashukuru sana na naipongeza Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siku nne zilizopita tulikuwa na sakasaka na hekaheka kule Sengerema kwenye kivuko cha Kamanga. Mheshimiwa Waziri nakushukuru sana pamoja Mheshimiwa Naibu Waziri na Watendaji wako kwa kutatua hilo tatizo na sasa vivuko vyote vinafanya kazi, kwa hiyo nashukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kule kwangu nimetengewa fedha za matengenezo ya barabara lakini nataka nimkumbushe Mheshimiwa Waziri nafahamu kwamba hii ni bajeti ya kwanza kama walivyozungumza Wabunge wengine, siyo rahisi sana mambo yote yaliyoahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi na hata kwenye mipango yetu yakawa reflected kwenye bajeti hii. Nonachoomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kufanya majumuisho asisahau kuzungumzia barabara ya Kangama - Sengerema kilometa 35 ambapo ukisoma Ilani ya Uchaguzi, ukurasa wa 60 utaona imehaidiwa kujengwa kwa lami. Pia kuna barabara nyingine ya Sengerema – Nyehunge, Jimbo la Buchosa kwa Mheshimiwa Dkt. Tizeba, kilometa 68 iko kwenye ahadi. Tuna barabara nyingine ya kutoka Busisi, Jimbo la Sengerema kwenda Jimbo la Nyang‟hwale na kuelekea Msalala hadi Kahama kwenye Jimbo la Mheshimiwa Maige. Hii ni barabara ambayo imeahidiwa na Mheshimiwa Rais kujengwa kwa lami. Ni barabara inayounganisha mikoa mitatu, mkoa wa Mwanza, Geita pamoja na Shinyanga. Naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kufanya majumuisho azungumzie hilo pia kutupa matumaini kwamba mipango ya utekelezaji itafanyika lini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la reli limezungumzwa sana na hasa nazungumzia reli ya kati. Kitu ambacho nataka niseme, hizi hotuba zinavyokuja hapa zina miongozo yake, hotuba tunazozijadili hapa zinaletwa kwa miongozo. Mojawapo ya mazingatio ambayo hotuba hizi zinatakiwa kuyazingatia ni Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa sababau ndiyo Serikali iliyoko madarakani lakini pia na ahadi na maagizo au maelekezo ya wakuu wa Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nazungumzia ujenzi wa reli ya kati, jambo hili siyo jipya wala siyo geni, tumelizungumza kwenye Mpango wa Maendeleo, tumelizungumza katika mazungumzo yetu ya kawaida na pia tumekuwa tukizungumza katika bajeti zilizopita. Kwenye Ilani yetu unafahamu, ukisoma ukurasa wa 66, ahadi ya 69 utaona tumesema upembuzi yakinifu ulishakamilika, kwa hiyo ilikuwa ni kwenda sasa kufanya upembuzi wa kina zaidi ili hatimaye ujenzi uanze na kikwazo kikubwa ilikuwa fedha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nazungumza hili kwa uchungu kwa sababu inavyokuja ni kama vile ujenzi wa reli ya kati haujawekwa wazi hapa. Ukisoma ukurasa wa tano na wa sita wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri inasema, hotuba hii imetayarishwa kwa kuzingatia Ilani ya uchaguzi, mambo mengine pamoja na maagizo ya Serikali. Tarehe 25 Aprili, Serikali kupitia Msemaji wa Ikulu, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano…
NAIBU SPIKA: Kengele ni moja Mheshimiwa Ngeleja, dakika tano zimekwisha.
MHE. WILLIAM M. NGELEJA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, nakushukuru sana.