Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ili niweze kuchangia bajeti ya Waziri wa Fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru na nampongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mambo anayoyafanya sana miradi anaisimamia na ametoa hela nyingi kwenye bajeti hii. Ni kweli bajeti hii imemgusa kila mmoja kwenye kila nyanja kweli tunamshukuru Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ninapoanza kuchangia nianze na ukusanyaji wa mapato. Naomba sana Serikali inakusanya mapato na ina njia ambayo imetumia ya kukusanya mapato lakini nilikuwa nashauri kuwa ifanye utafiti mzuri ambao utaweza kukusanya mapato. Mimi ni mmojawapo nikienda dukani kununua kitu naomba risiti, mmoja mmoja atakupa risiti lakini wengi watakuambia kuwa EFD machine zimeharibika hazifanyi kazi, kwa hiyo unakuta Serikali tunapoteza sana mapato kwa kutodai risiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu, kuna viongozi wengi ambao wako Wilayani, ambao wako Mkoani, ambao wako kwenye Halmashauri naamini tukiwa-task waweze kufuatilia Maafisa Biahsara wataweza kufuatilia na kuwachukulia hatua hao wafanyabiashara ambao hawataki kutoa hela zetu kusudi tuweze kupata mishahara pamoja na wale watu wafanyakazi waweze kupata mishahara yao pamoja na miradi ya maendeleo iweze kutimilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuwa mapato tunapata lakini kuna Wakandarasi, Wakandarasi kwa kweli wana shida wanafanya kazi zao lakini hawalipwi. Kwa hiyo, nilikuwa nashauri Mheshimiwa Waziri wa Fedha waangalie hawa Wakandarasi wanaishi maisha mabaya na huku wameshafanya kazi. Kwa hiyo, naomba muwaangalie walipwe hela zao ili kusudi waweze kuendelea na kazi zingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naongelea kuhusu asilimia kumi ya mapato ya Halmashauri. Hii asilimia 10 ambayo akina mama pamoja na vijana pamoja na wenye ulemavu ambayo wanatengewa ni nzuri sana, lakini kwa sababu ya changamoto Serikali imesema kuwa bado wanaifanyia kazi. Naomba na ninashauri kuwa kwa sababu ni jambo muhimu sana ambalo linawakomboa sana hasa wanawake wakiwepo na wanawake wa Morogoro na wanawake wote waliokuwa wanapata mikopo hii, naomba muifanyie haraka sana kusudi tuweze kupata ufumbuzi wake, waweze kuendelea na mikopo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo naongelea ni reli ya mwendokasi. Naipongeza Serikali nampongeza Mheshimiwa Rais kwani anafanya mambo mazuri sana. Tumeambiwa kuwa kipande cha Dar es salaam mpaka Morogoro ambacho kina kilomita 300 karibu kinakamilika kina asilimia 98.14 ambayo sasa hivi kinakamilika na mabehewa ninyi mmeyaona mabahewa ya ghorofa ambayo yameletwa, vichwa ambavyo vimeletwa naaamini kuwa hivi karibuni na kama sikosei labda mwezi ujao kipande cha Dar es salaam mpaka Morogoro kitaanza safari zake. Kwa hiyo, naomba na ninatoa ushauri kwa wananchi ambao watatumia hii reli waitunze, tuzidi kuitunza kusudi iweze kuendelea vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye barabara, Mheshimiwa Rais ameunganisha barabara, Mkoa kwa Mkoa na ameunganisha mpaka nchi yetu na nchi jirani. Kwa hiyo, licha ya kumpongeza naomba barabara ya kuanzia Kibaha hadi Morogoro ambayo ina njia nne ingawaje imefanyiwa usanifu, hela zikitengwa iweze kukamilika kwa ni kuna foleni ya malori. Nanyi ni kweli mnasafiri kwenye barabara hii mnaiona hiyo foleni ya malori inavyosumbua, kwa hiyo naomba sana hiyo barabara kwenye bajeti hii iweze kufanyiwa kazi ili kusudi tuweze kupata usafiri ambao unaeleweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna barabara ambayo huwa tunaisemea mara kwa mara ya Bigwa mvua inakwenda kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere, tunayo barabara tunaisema Ubena - Zomozi mpaka kwenda mpaka Bwawa la Mwalimu Nyerere ndiyo kwenye mpango ilikuwepo, lakini naomba itengenezwe kwa sababu ni muda mrefu tumeiongelea hii barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu kilimo. Kilimo kinaajiri wananchi ambao ni asilimia 65.5 na zaidi. Kwa hiyo, kilimo ukitaka watu waweze kutoka kwenye umaskini ni sekta za uzalishaji ambazo sekta za uzalishaji ni kilimo. Kwa hiyo, kilimo namaanisha uvuvi, mifugo ambazo zinaweza kuwakomboa wananchi. Kwa hiyo, fedha zilizotengwa huko huko wakati mwingine tunatenga fedha hazitoki, kwa hiyo, tutakapopitisha hiyo bajeti naomba fedha tutakazozitenga zitoke na hasa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji kutokana mabadiliko ya tabianchi ambacho kitaweza kumkomboa mwananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na nampongeza Mheshimiwa Rais kwa bajeti ambayo imetengwa ambayo tunaiongelea sasa hivi bilioni 98.8 kitu kama hicho, hiyo bajeti ni kubwa sana. Bilioni 970.8 ambayo ndiyo bajeti ya kilimo, naamini ni kubwa sana ikisimamiwa vizuri sana itaweza kumkomboa mwananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa angalizo kuwa hiyo hela ambayo imetengwa naomba kadri bajeti zinapokuja hizi zinazokuja mbele mwaka kwa mwaka tuweze kupata bajeti zaidi ya hii ili tuweze kufikia Azimio la Malabo na Maputo ambayo ni asilimia kumi ya bajeti nzima iende kwenye kilimo. Kwa hiyo, naamini Mheshimiwa Rais anayependa kilimo na kukipa kipaumbele naamini atafanya hivyo, Mama ni mzuri Mama anafanya vitu vizuri anafanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu mazingira. Nampongeza sana Mheshimiwa Makamu wa Rais kwa kuisimamia hiyo kampeni ya kupanda miti. Naomba sana wananchi, itaendelea kutenga fedha zinazotengwa kwa mambo ya Maliasili na Mazingira, tuweze kusimamia hiyo miti tuipande ambayo kila Halmashauri, kila Wilaya ni 1,500,000 inapandwa lakini ikipandwa tuweze kuifuatilia kuwa kweli inastawi na haikauki, hayo tunaweza kwa sababu ya mazingira. Pia licha ya kupanda miti tumehamasisha, wanahamasishwa, tuwahamasishe wananchi waweze kutumia nishati mbadala hasa kwa kupika, ili kusudi tuweze kupunguza kutumia mikaa pamoja na kuni tuweze kwenda vizuri kutunza mazingira yetu na yatatutunza naamini tukiweza kutunza haya mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu elimu. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais, tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa mambo inayofanya ambayo ni wanafunzi wetu watasoma mpaka kidato cha sita bila ya malipo ya school fees, pia imetoa mambo ya vyuo vya kati itayafanyia vizuri sana. Pia na Vyuo Vikuu inatoa mikopo ya kutosha kwa hiyo naamini itaendelea kutoa mikopo kwa kila mwanafunzi kwa sababu hapo baadae wataweza kurudisha mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu umeme, tunashukuru Serikali yetu, ni kweli watu walikuwa hawajui umeme lakini miaka hii umeme umesambaa kila mahali na tunaamini tunakwenda kwenye vitongoji kila mmoja anayeweza kuweka umeme kwa shilingi 27,000 huko vijijini ataweza kuweka umeme. Kwa hiyo, tunampongeza mama anafanya kazi kubwa. Lakini naomba kuna Kata za Morogoro, Mgeta, Tarafa ya Mgeta ambayo bado Kata nzima vijiji vyote Kata kama nne hazijapata umeme. Kwa hiyo nashauri, namuomba Mheshimiwa Waziri anayehusika, aweze kuliona hilo jambo kuwa vijiji vyote vya Kata nzima havina umeme, Kata, Tarafa ya Mgeta vijiji vya Kata nne na zingine kwenye Wilaya ya Mvomero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisemee kuhusu barabara. Barabara za Mkoa wa Morogoro hasa za vijijini zikiwepo zinazosimamiwa na TARURA naomba ziangaliwe. Nakuomba sana ziweze kuangaliwa ziweze kutengenezwa ziweze kukamilika watu wa TARURA waweze kuona wana jukumu la kuweza kuona hizo barabara zinatengenezwa kwa sababu tuweze kwenda vizuri maendeleo ni maendeleo namshukuru Mama Samia namshukuru Rais wetu anatupenda na sisi tumpende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nakushukuru na nasema ubarikiwe na Mwenyezi Mungu, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)